Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 217 | 2025-05-05 |
Name
Vincent Paul Mbogo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nkasi Kusini
Primary Question
MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza:-
Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Vituo vya Polisi, Kata za Kate na Kipande, kwani tayari maeneo yameandaliwa?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Kate umefikia kwenye hatua ya umaliziaji na kiasi cha fedha, shilingi 25,000,000, kimetengwa kwenye Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Katika Kata ya Kipande limetengwa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 8,092 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Kata, utakaogharimu shilingi 115,000,000. Fedha hizo zitatengwa kwenye mwaka wa fedha 2026/2027. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved