Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Finance | Wizara ya Fedha | 216 | 2025-05-05 |
Name
Muharami Shabani Mkenge
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bagamoyo
Primary Question
MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kusitisha kutoa vibali kwa mashine za Kamari ili kupunguza umaskini kwa Vijana?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la waendeshaji mashine za slots pasipo kuzingatia sheria za michezo ya kubahatisha na sheria nyingine za nchi. Mathalani, waendeshaji haramu huweka mashine zao kwenye makazi ya watu, maduka ya bidhaa, maeneo ya vijijini na pia huruhusu watu wa chini ya miaka 18 kushiriki katika michezo hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na changamoto hizi, bodi imechukua hatua kadhaa kama ifuatavyo: -
(i) Kusitisha utoaji wa leseni kwa waendeshaji wapya wa mashine za sloti;
(ii) Kuanzisha misako na operation ya kusaka waendeshaji haramu wa mashine za sloti nchi nzima kwa kushirikiana na mamlaka nyingine kama vile Polisi, TRA na Uhamiaji;
(iii) Kuongeza kaguzi za mara kwa mara katika maeneo mbalimbali ya nchi ilipo biashara ya mashine za sloti;
(iv) Kuendesha kampeni inayowalenga vijana na jamii kufanya kazi za uzalishaji;
(v) Kuongeza udhibiti wa uingizaji wa mashine za sloti hapa nchini kwenye maeneo ya mipakani kwa kushirikiana na TRA;
(vi) Kuanza mchakato wa kutumia mifumo ya kielektroniki kudhibiti biashara ya mashine za sloti zinazoendeshwa mitaani;
(vii) Kuingia makubaliano (MoU) na Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa lengo la kuwa na ushirikiano wa karibu wa kudhibiti waendeshaji haramu wa mashine za sloti; na
(viii) Kupitia mara kwa mara Sheria ya Michezo ya Kubahatisha kwa lengo la kuondoa kasoro na mianya inayotumiwa na waendeshaji haramu wa mashine za sloti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi inakusudia kutekeleza hatua hizi kikamilifu ikiwa ni sehemu ya juhudi yake ya kuhakikisha kuwa, jamii ikiwemo vijana inalindwa dhidi ya athari hasi za michezo ya kubahatisha ikiwemo umaskini. Bodi itaendelea kuchukua hatua zaidi za kuondoa athari zote hasi za michezo ya kubahatisha. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved