Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Finance and Planning | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 213 | 2025-05-05 |
Name
Saashisha Elinikyo Mafuwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Hai
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:-
Je, lini Serikali italipa madeni ya Walimu wa Shule za Sekondari waliohamishiwa Shule za Msingi?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kuboresha ikama ya walimu wa shule za msingi nchini imekuwa ikihamisha walimu kwa kuzingatia ikama ya Halmashauri husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipindi cha mwaka 2017 hadi 2025, walimu 1,914 wamehamishwa kutoka shule za sekondari kwenda shule za msingi. Fedha iliyohitajika kwa ajili ya uhamisho huo ni shilingi bilioni 2.08 ambapo shilingi bilioni 1.22 zimelipwa na kiasi ambacho hakijalipwa ni shilingi milioni 865.93. Serikali itaendelea kulipa madeni ya uhamisho wa walimu kadri ya upatikaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved