Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 212 | 2025-05-05 |
Name
Joseph Anania Tadayo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwanga
Primary Question
MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza:-
Je, Serikali kupitia TARURA ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Barabara ya Mangio hadi Kivizini Wilayani Mwanga?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Mangio hadi Kivisini yenye urefu wa kilometa 7.1 inapatikana ukanda wa milimani katika Wilaya ya Mwanga. Kwa sasa TARURA inaendelea na usanifu wa barabara hiyo ambapo utakapokamilika na makisio ya gharama kufahamika itawekwa kwenye mipango ya bajeti kwa ajili ya utekelezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuhudumia mtandao wa barabara na madaraja katika Wilaya ya Mwanga kwa kujenga, kukarabati na kufanya matengenezo kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved