Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 210 | 2025-05-05 |
Name
Stella Simon Fiyao
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:-
Je, kwa nini Wastaafu hawapewi haki zao mara tu wanapostaafu?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ucheleweshaji wa malipo ya mafao ya wastaafu katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa sasa limekuwa historia. Mifuko imeboresha mifumo yao ya TEHAMA, hatua ambayo imeiwezesha kulipa mafao ya wastaafu ndani ya kipindi kilichowekwa kisheria, au hata kwa muda mfupi zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kusimamia kwa karibu utendaji wa Mifuko ili kuhakikisha kuwa inaendelea kuondoa vikwazo na kuwalipa wastaafu mafao yao mapema kadri inavyotakiwa. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved