Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 35 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 454 | 2025-05-29 |
Name
Leah Jeremiah Komanya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Meatu
Primary Question
MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Bwawa katika Kijiji cha Lukale na Mwabagimu Wilayani Meatu ili kuondakana na adha ya maji ya chumvi?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ruhusa yako, ninaomba nitumie nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, viongozi wote wa Serikali, chama, Bunge lako Tukufu, ukiwepo wewe pamoja na Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wabunge, Wananchi wa Jimbo la Pangani na Watumishi wote wa Wizara ya Maji. Tumepitia kipindi kigumu cha kuondokewa na mdogo wangu kipenzi, Ally Hamidu Aweso, nikiwa katika shughuli zangu za Bunge. Mungu anasema, “Yapaswa kushukuru kwa kila jambo.” Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa mtihani huu mzito, lakini Mungu ailaze mahali pema Peponi roho ya Marehemu. Amina.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa muda mfupi, Serikali imekamilisha ujenzi wa bwawa dogo katika Kijiji cha Lukale, Wilayani Meatu, ambapo kupitia bwawa hilo, wananchi wanapata huduma ya maji kwa kutumia pampu ya mkono. Aidha, katika hatua nyingine, Serikali imeanza hatua za awali za ujenzi wa mabwawa ya maji katika Vijiji vya Lukale na Mwabagimu, ambapo kazi zinazofanyika kwa sasa ni utafiti wa udongo na upembuzi yakinifu ili utekelezaji wake uweze kuanza.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved