Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 35 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 452 | 2025-05-29 |
Name
Joseph Michael Mkundi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Primary Question
MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Tawi la Chuo cha Uuguzi na Uganga - Ukerewe?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli. Bado kuna mahitaji ya vyuo katika maeneo mbalimbali ya nchi, ila kwa sasa Serikali inajenga hospitali yenye hadhi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa katika Wilaya ya Ukerewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na ujenzi huo, Serikali itaendelea kufanya upembuzi yakinifu kuona kama eneo hilo litahitaji kuwa na Chuo cha Uuguzi mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved