Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 35 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 450 | 2025-05-29 |
Name
Justin Lazaro Nyamoga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilolo
Primary Question
MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: -
Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha CBE katika Kata ya Lugalo – Kilolo?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kilikabidhiwa eneo rasmi, Hati ya umiliki wa eneo la Chuo, Wilaya ya Kilolo mnamo tarehe 8 Julai, 2024 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia CBE inaandaa Mpango Kabambe (Master Plan) kwa ajili ya uendelezwaji wa kudumu wa Kampasi hiyo. Aidha, baada ya kukamilika kwa mpango kabambe, ujenzi wa Chuo kwa Kampasi ya Iringa iliyopo Kata ya Lugalo katika Wilaya ya Kilolo utaanza rasmi 2025/2026 kadri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved