Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 35 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 449 | 2025-05-29 |
Name
Eng. Stella Martin Manyanya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nyasa
Primary Question
MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:-
Je, hatua gani imefikiwa kupeleka umeme Kitongoji cha Songea Pori na Nindi vinavyopakana na Msumbiji kama ilivyoahidiwa na Serikali?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Kitongoji cha Songea Pori kilichopo katika Kijiji cha Lunyele, Kata ya Mpepo na Kitongoji cha Nindi kilichopo Kijiji cha Konganywita, Kata ya Mipotopoto vilifanyiwa upembuzi yakinifu na kubaini kwamba, vinahitaji kuwekewa njia za kusambaza umeme za msongo wa kati kwa umbali wa kilometa tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatarajia kuvipelekea umeme vitongoji hivi kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili “B” ambao utekelezaji wake utaanza mwaka huu wa fedha 2025/2026. Kwa sasa taratibu za kuwapata wakandarasi zinaendelea, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved