Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 35 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 448 | 2025-05-29 |
Name
Ally Juma Makoa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kondoa Mjini
Primary Question
MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Kondoa Mjini?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Kondoa Mji ina mahitaji ya walimu 674 (msingi 414 na sekondari 260), waliopo ni 450 (msingi 266 na sekondari 184) na upungufu ni walimu 224 (msingi 148 na sekondari 76).
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2024/2025 Serikali imeajiri walimu 15,925 wa shule za msingi na shule za sekondari ambapo Halmashauri ya Kondoa Mji ilipangiwa walimu 33 (msingi saba na sekondari 26).
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuajiri walimu na kuwapangia vituo vya kazi katika maeneo yenye uhitaji mkubwa. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved