Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nassoro Rashid Nassoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. NASSORO RASHID NASSORO aliuliza: - Je, lini Serikali itaweka kituo kidogo cha uhamiaji katika eneo la Makangale linalokua kwa kasi kiutalii kwa ajili ya ukaguzi wa wageni?

Supplementary Question 1

MHE. NASSORO RASHID NASSORO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri aliyonipa, lakini katika eneo hilo la Makangale ambalo sasa hivi linaendelea kukua kiutalii na wageni wanaingia na kutoka, na wengine bila kuripoti katika Ofisi za Uhamiaji. Juzi tu kuna mgeni tulimkamata ana wiki mbili hajaripoti katika Ofisi za Uhamiaji na tukaweza kumpeleka katika Ofisi za Uhamiaji. Je, Waziri ana mpango gani kwa sasa hivi kuweza kuidhibiti hiyo hali au kuiondoa kabisa?

Name

Kaspar Kaspar Mmuya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kumshukuru Mheshimiwa Nassoro Rashid Nassoro, kwanza kwa uzalendo wa kujua na kuifanyia kazi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hususan kwa kuwa mlinzi wa eneo ambalo unatoka.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili naomba nikuhakikishie kuwa eneo hilo ni la kimkakati, ni kati ya shehia ambazo zipo kwenye eneo ambalo watalii wengi sana wanakuja. Nikuhakikishie kwamba nitaongeza idadi ya askari ambao watakuja kushirikiana na viongozi wote wa shehia ili kuweza kufanya doria na kuimarisha vipenyo vyote ambavyo kuna uwezekano wa hao wanaokuja kuingia na kutoka bila kufuata utaratibu.

Mheshimiwa Spika, pia tutaendelea kuwachukulia hatua wote ambao watapatikana kadri ya vile ambavyo itathibitika kuwa wameingia na kutoka bila kufuata utaratibu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Amosy William Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. NASSORO RASHID NASSORO aliuliza: - Je, lini Serikali itaweka kituo kidogo cha uhamiaji katika eneo la Makangale linalokua kwa kasi kiutalii kwa ajili ya ukaguzi wa wageni?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Sikonge ni miongoni mwa wilaya za zamani, lakini mpaka hivi sasa hatuna Ofisi ya Uhamiaji. Hivi sasa watendaji wa Ofisi hii ya Uhamiaji wapo katika kijumba kidogo sana na wanafanya kazi katika mazingira magumu kweli. Je, ni lini sasa Serikali itaona haja ya kwenda kujenga kituo cha Uhamiaji katika Wilaya ya Sikonge? Ahsante sana.

Name

Kaspar Kaspar Mmuya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuimarisha miundombinu ya utoaji huduma kwa Askari wa Idara hii ya Uhamiaji, hususankwenye upatikanaji wa Ofisi za Mkoa na Wilaya.

Mheshimiwa Spika, naomba nikuhakikishie, bajeti ya 2026/2027 moja kati ya vipaumbele vyake ni kuweka bajeti kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hizi. Sasa katika Wilaya ya Sikonge ninaomba tuipe kipaumbele kwa ajili ya upatikanaji wa ofisi hiyo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.