Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Mwamengo Ulimboka Baraka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyela
Primary Question
MHE. BARAKA A. U. MWAMENGO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Ibanda – Kiwira Port kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 1
MHE. BARAKA A. U. MWAMENGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza, na ninashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipande hiki cha Barabara cha kutoka Ibanda kwenda Itungi Port kwa sasa kimeharibika sana na hasa section ya kutoka Kyela Mjini mpaka Itungi Port na Wananchi wa Kajunjumele wanapata shida sana. Je, Waziri atakuwa tayari kufika Kyela kutembelea hicho kipande ili kuweza kujionea hali iliyopo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, niishukuru Serikali kwa jinsi ilivyotoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Border Post pale Kasumulu kwenye mpaka wetu na Malawi. Ninaishukuru sana Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia. Je, Serikali itakuwa tayari kutoa fedha za kujenga barabara inayounganisha ile Border Post ya Kasumulu ili kuonesha nia njema ambayo Mheshimiwa Dkt. Samia ametoa fedha kwa ajili ya kile kituo cha border ya pamoja ikiwemo barabara za kuingia stendi na taa za kufanana na kile kituo kilichojengwa, kile cha border ya Kasumulu? (Makofi)
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ikishakuwa na mkandarasi, mara nyingi mkandarasi ndiye anahusika, kwa hiyo, nina uhakika kwa kuwa alisimamishwa, kutakuwa kuna mahitaji makubwa yanahitajika ya kutengenezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninaomba tu kutumia Bunge hili Tukufu kumwelekeza Meneja wa Mkoa wa Mbeya ambapo nilisikia wanamsifia sana, na kweli ni mchapakazi mzuri, aweze kuwasiliana na TANROADS Makao Makuu, kwa kuwa mkandarasi hayupo, basi aweze kupata fedha ya dharura ya kuitengeneza barabara hiyo iweze walau kupitika na kuondoa hiyo adha kwa sababu mkandarasi hayupo kwa muda mrefu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kufanya matengenezo ama ujenzi wa barabara ya kwenda stendi na kuweka taa kwenye ile eneo la OSBP ili kupata sura nzuri ya nchi; ninajua hiyo ndiyo sehemu ambayo wananchi wetu wanapokwenda Malawi, ndiyo njia ya kutokea, na pia wananchi wa kutoka Malawi ndipo wanapoingilia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwelekeze Meneja wa Mkoa wa Mbeya aweze kuangalia hizi barabara, afanye tathmini na kuleta mahitaji. Nina uhakika atashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kuona nini wangetamani kifanyike katika ile OSBP ambayo ndiyo mpaka wa kwenda Malawi, waangalie namna ya kuboresha halafu walete tathmini tuweze kutafuta fedha, na kufanya watu wanapoingia katika nchi yetu kuwe na sura ambayo wanasema sasa wanatoka Malawi, wanaingia Tanzania.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved