Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Zuberi Yahya Mfaume
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini
Primary Question
MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:- Je, lini Serikali itaingilia kati na kudhibiti migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wawekezaji wa Morogoro Sugar?
Supplementary Question 1
MHE. ZUBERI Y. MFAUME: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza na nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Hata hivyo, nimweleze kwamba kuna changamoto kubwa katika eneo la Bwakila Chini, kwa maana ya Kijiji cha Ngwade, Serikali imepima maeneo kwa ajili ya kuwamilikisha wananchi na wananchi wamelipa fedha zote, lakini hadi sasa hawajapatiwa hati zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo katika Kijiji cha Msonge pia wananchi walijiunga katika kikundi kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kilimo, wakawa na makubaliano na Serikali ya kujenga zahanati katika eneo husika, wananchi hawa waliahidiwa kupimiwa viwanja na Wizara ya Ardhi na kumilikishwa na tayari wamefanya wajibu wao kwa kujenga jengo lile, lakini hadi sasa Serikali haijatimiza wajibu wake wa kuwapimia na kuwapatia hati ili waendeleze shughuli za kilimo katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari sasa kuambatana nami jimboni kuwasikiliza wananchi na kujionea changamoto hizi ili aweze kuzitolea majibu? Ninafahamu Mheshimiwa Naibu Waziri kwa muda mchache aliohudumu katika ofisi yake ni bingwa wa utatuzi wa migogoro ya ardhi, ahsante.
Name
Kaspar Kaspar Mmuya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ruangwa
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza Morogoro Kusini kwa kweli wamechagua Mbunge ambaye anafuatilia changamoto mbalimbali za wananchi wake. Wakati ni mgeni kabisa katika nafasi hii alishawahi kunipigia na tuliwahi kuzungumza juu ya changamoto mbalimbali na hatma yake na leo hii ameleta jambo hili na anazidi kuwatetea kujua haki ambazo wanastahili katika maeneo hayo, hongera sana Mbunge na hongereni wananchi wa Morogoro Kusini kwa kupata mwakilishi mzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji alivyovitaja na alivyozungumza kuhusu haki yao ya kupatiwa hati, huo ni wajibu wa Wizara kwa sababu tayari mpango ulishapangwa na upimaji umeshafanyika, ni suala la kutoa hati tu. Nikuahidi, nitaambatana na wewe katika ziara ambayo tutakubaliana, tutaenda maeneo husika na siku hiyo nikuhakikishie kama kutakuwa na hati ambazo wanastahili kupewa watu hao katika vijiji hivyo tutazitoa na wewe ukiwemo na wananchi wako wote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved