Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jamal Ramadhan Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbwini

Primary Question

MHE. MWINYI JAMAL RAMADHAN aliuliza:- Je, kwa nini Bandari ya Dar es Salaam inashindwa kupokea meli nyingi kwa wakati mmoja?

Supplementary Question 1

MHE. MWINYI JAMAL RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa heshima hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa bandari hii ni bandari tegemezi kwa wafanyabiashara wetu kutoka visiwani na bara na inaleta tija sana kwa uchumi wa nchi yetu, swali langu lipo hapa, ni mara ngapi tangu nchi yetu imepata uhuru bandari hii imefanyiwa utanuzi ama ujenzi wa kuongezwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la nyongeza, katika jitihada za Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukuza uchumi wetu wa nchi na kuweka mkazo katika eneo hili, hatuoni sasa suluhisho la kuongeza uchumi wa nchi yetu ni kwa kutengeneza Bandari ya Bagamoyo? Sambamba na hilo, tujue, je, Bandari ya Bagamoyo kwa sasa imefikia wapi?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Jamal Ramadhan kwa uzalendo wake mkubwa wa kufuatilia miundombinu ya kimkakati katika Taifa letu hususan roho ya nchi ambayo ni bandari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia uhuru kwa kweli takwimu specific nitashindwa kuzisema hapa lakini ni mara ngapi Serikali imefanya maboresho? Ni mara nyingi katika kuhakikisha na kuona kwamba bandari hii inaongezewa uwezo. Pamoja na mambo ambayo yamefanyika huko nyuma, bado inaendelea kufanya hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tumeboresha gati namba sifuri mpaka namba saba ambapo imeongeza uwezo wa bandari yetu kuhudumia. Pia tumeongeza kina cha bandari yetu ili iweze pengine kuwa na urefu zaidi kwenda chini pamoja na kuongeza upana wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, tuna miradi mingine inayoendelea bandarini, kama vile kuunganisha reli kwenye bandari yetu, kuhakikisha kwamba tunajenga Gati Namba 12 mpaka 15, kama nilivyozungumza kuhakikisha kwamba, tunawezesha Kituo chetu cha Kurasini kinakuwa na uwezo mkubwa wa kuhudumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, tayari kuna mradi mkubwa ambao uko 32%, mradi wa kujenga matenki 15 yenye uwezo wa kuhifadhi mita za ujazo wa mafuta 378. Maboresho yote hayo yana lengo moja tu la kuhakikisha kwamba, bandari yetu inazidi kuimarisha uwezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, swali lake la pili la nyongeza ametaka kufahamu kuhusiana na ujenzi wa bandari yetu ya Bagamoyo ya Mbegani. Ni kweli kabisa ukiangalia uwezo wa mahitaji yetu sasa ya mzigo kutokana na diplomasia nzuri ya Rais wetu, na jinsi anavyosimamia Uchumi, unaona kabisa Bandari ya Dar es Salaam hata ungeifanyia maboresho kiasi gani inazidi kuzidiwa. Hivyo basi, Serikali imefanya maamuzi ya kuboresha au kuanza ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, Mbegani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyozungumza, tumeshamaliza usanifu. Tayari tumeanza taratibu kwa ajili ya kuanza ujenzi, ili tuanze na kilomita moja, kwa ajili ya kupata kilomita 1.3, kupata gati ambayo itawezesha sasa meli kubwa ambazo kwa sasa haziwezi kutua kwenye Bandari ya Dar es Salaam, ambayo itakuwa inaweza kufika pale. Kwa kweli, bandari ile ikianza kufanya kazi itakuwa ndiyo bandari kubwa kuliko zote kwa ukanda wetu wa Afrika.

Name

Dr. Regina Christopher Malima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWINYI JAMAL RAMADHAN aliuliza:- Je, kwa nini Bandari ya Dar es Salaam inashindwa kupokea meli nyingi kwa wakati mmoja?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. REGINA C. MALIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Nina swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri kuhusiana na Bandari ya Nansio katika Kisiwa cha Ukerewe. Bandari hii pia, imechakaa, imechoka, haijawahi kufanyiwa ukarabati tangu uhuru. Wakati mwingine hali ya hewa ikiwa ni mbaya meli pia zinapata shida kuweza kupaki. Kwa hiyo, ninaomba kujua, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Bandari hii ya Nansio katika Kisiwa cha Ukerewe? Ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka anapoingia madarakani Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwaka 2021, takribani bandari 80 zilikuwa zinatambuliwa na kurasimishwa. Kutokana na umuhimnu wa sekta ya bandari, Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo maalumu na mahususi kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Wizara ya Uchukuzi kwanza, tufanye urasimishaji. Tumekamilisha urasimishaji na bandari zimeongezeka mpaka 142.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili ni kuanza kutafuta fedha, kuboresha bandari moja baada ya nyingine. Namwomba Mheshimiwa Malima awe na Subira, Bandari ya Nansio ni moja kati ya bandari muhimu kwenye Taifa letu. Tutakwenda kuifikia pindi fedha zitakapokuwa zimepatikana.