Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Moses Charles Bujaga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sumve
Primary Question
MHE. MOSES C. BUJAGA aliuliza:- Je, lini Serikali itatimiza ahadi ya ujenzi wa Vituo vya Afya Walla, Mwambomba, Mwagi, Mhandi na Mwamala?
Supplementary Question 1
MHE. MOSES C. BUJAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, ningependa kuongeza maswali madogo mawili. Kituo cha Afya Budushi kina daktari mmoja, Kituo cha Afya Kadashi kina daktari mmoja, na Kituo cha Afya Isunga hakuna daktari. Ningependa kujua Serikali ina mpango gani wa dharura kuhakikisha kwamba tunapata watalamu katika vituo hivi vitatu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kituo cha Afya Budushi hakina gari la kubeba wagonjwa inapotokea dharura ya kupeleka wagonjwa hao kwenye Hospitali ya Wilaya iliyoko kilometa 33. Je, Serikali itatupatia lini gari la kubeba wagonjwa Kituo cha Afya Budushi? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuuliza maswali mawili ya nyongeza na ninaomba niyajibu kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu upungufu wa madaktari na ndiyo maana tulipata vibali vya kuajiri madaktari 5,000 nchi nzima na baadhi ya madaktari wameshafika maeneo yao ya kazi. Ninawaomba madaktari waliopangiwa kwenda kwenye vituo vyetu vya afya ili wafike kwa wakati, lakini kama haitoshi nimwelekeze Mkurugenzi kuendelea kutoa ajira zile za lazima hasa kwenye maeneo ambayo tuna upungufu kama alivyoainisha Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu magari ya kubebea wagonjwa, tayari tulishapeleka magari zaidi ya 594 katika maeneo yetu kwa Halmashauri zote nchini, lakini pia tunaendelea kuomba magari. Kadiri tunavyoyapokea kutoka Wizara ya Afya, tutaendelea kuyaelekeza katika vituo vyetu vya afya. (Makofi)
Name
Sylivia Francis Sigula
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MOSES C. BUJAGA aliuliza:- Je, lini Serikali itatimiza ahadi ya ujenzi wa Vituo vya Afya Walla, Mwambomba, Mwagi, Mhandi na Mwamala?
Supplementary Question 2
MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kata ya Ilemba iliyoko Wilaya ya Sumbawanga DC yenye wakazi zaidi ya 27,000 haina Kituo cha Afya, na nimekuwa nikiuliza swali hili, na majibu ya Serikali yamekuwa ni yale yale. On a serious note, ni lini hasa ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ilemba utaanza? (Makofi)
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Sylvia kwa kuuliza swali hili la nyongeza. Nimhakikishie ya kwamba Wilaya ya Sumbawanga DC kwa kata aliyoiainisha Mheshimiwa Mbunge, nimhakikishie tunakwenda kujenga Kituo cha Afya na kitaanza kutoa huduma kwa watu wetu. Serikali ya awamu hii siyo ya busness as usual, tunakwenda kufanya hakika. Niwahakikishie wananchi wa Kata hii watapata huduma ya afya. (Makofi)
Name
Tinnar Andrew Chenge
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MOSES C. BUJAGA aliuliza:- Je, lini Serikali itatimiza ahadi ya ujenzi wa Vituo vya Afya Walla, Mwambomba, Mwagi, Mhandi na Mwamala?
Supplementary Question 3
MHE. TINNAR A. CHENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kuniona. Kwa niaba ya wanawake wa Mkoa wa Simiyu, ninaomba kuulizwa swali la nyongeza. Ni lini Serikali ina mpango wa kujenga Kituo cha Afya cha Bunamhala Wilaya ya Bariadi?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza kuhusu Kituo cha Afya Simiyu, Bariadi. Katika vile vituo vyetu vya kimkakati Majimbo 94 na yale Majimbo mapya pamoja na Halmashauri ya Wilaya Simiyu na wao ni wanufaika, watakwenda kupata kituo cha afya. (Makofi)
Name
Anne Kilango Malecela
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Same Mashariki
Primary Question
MHE. MOSES C. BUJAGA aliuliza:- Je, lini Serikali itatimiza ahadi ya ujenzi wa Vituo vya Afya Walla, Mwambomba, Mwagi, Mhandi na Mwamala?
Supplementary Question 4
MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaishukuru sana Serikali kwa kutujengea Vituo vya Afya viwili; Kituo cha Afya cha Miamba na Kituo cha Afya cha Mtii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vituo hivyo vyote viwili hakuna hata kimoja chenye wodi za kulaza wagonjwa. Je, Serikali itaanza lini kutujengea wodi hizi kwa sababu vituo vya afya ni vikubwa, vina kila kitu lakini wagonjwa hawana mahali pa kulala?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vyote vya kimkakati vilipoanza kujengwa tulielekeza shilingi milioni 250 ambazo bado hazitoshi, na tayari tumeshawaelekeza Wakurugenzi kuanza kutenga fedha, mapato ya ndani kujenga wodi ambazo zinatakiwa kutoa huduma katika vituo vyetu vya afya. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved