Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emanuel Qambaji Nuwas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Mradi wa Maji wa Dambiya?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa chanzo hiki cha maji cha Dambiya kina maji ya kutosha na kitakwenda kuhudumia zaidi ya vijiji 21, tuna mji wa Dongobesh ambao ni Makao Makuu ya Halmashauri, una hospitali ya halmashauri, una kituo cha afya na vilevile una shule za sekondari mbili na shule za msingi tano. Mji huu sasa hivi hauna maji na unapata mgao wa maji angalau mara mbili....

SPIKA: Mheshimiwa twende kwenye swali.

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS: Mheshimiwa Spika, swali langu la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani kuweza kuvuta maji kutoka chanzo hiki ambacho ni chini ya kilometa saba na matanki yapo katika mji huu ili kuweza kuwasaidia wananchi hawa ambao wana tatizo la maji na huduma ziweze kuendelea?

Mheshimiwa Spika, swali la pili la nyongeza. Tunao mradi katika Kijiji cha Qaloda Kata ya Dongobesh ambao sasa Kijiji hiki kina kaya 386 na mradi huu umekwama kwa zaidi ya miaka miwili, na una mabomba pale. Je, Serikali ina mpango gani kukamilisha mradi huu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Dkt. Emanuel, Mbunge wa Mbulu Vijijini. Ni kweli kabisa mradi huu ambao unatekelezwa wenye gharama ya shilingi bilioni 41.2 ambapo Serikali mpaka sasa imeshamlipa mkandarasi takribani shilingi bilioni tisa.

Mheshimiwa Spika, mradi utakapokamilika utaweza kuhakikisha kwamba vijiji 76 vya Mbulu Vijijini vitakuwa vimepata huduma ya majisafi na salama. Vilevile, katika vijiji ambavyo vimebaki, ndani ya nchi yetu kati ya vijiji 12,318 ni vijiji 1,575 tu ambavyo vimeshabaki, ambapo miradi zaidi ya 3,714 vyenye gharama ya shilingi trilioni 1.8 vimeshakamilika na miradi 878 inayoendelea yenye gharama ya shilingi trilioni 1.3.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, katika miradi inayoendelea pamoja na huu ambao amesema kwamba unasuasua, tunaenda kuhakikisha mradi huo unakamilika na wananchi wake wa Mbulu Vijijini wanapata huduma ya majisafi na salama.