Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salum Khamis Salim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. SALUM K. SALIM aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa haraka na wa kudumu wa kuzuia tembo kuvamia Vijiji vya Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. SALUM KHAMIS SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri, lakini kwa sababu suala la tembo katika Wilaya ya Meatu na Jimbo la Meatu limekuwa ni la siku nyingi na mkakati wake ni huu huu kila siku, na majibu ni hayo hayo, je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni kwamba, kuna sababu ya kuwa na azma kubwa ya kuwaondoa tembo ambao wanaishi maeneo ya watu kwa sasa? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaomba kumpongeza sana Mheshimiwa Salum kwa kuwa na yeye sasa ni sehemu ya hifadhi na anashirikiana na taasisi zetu katika kuhami jamii yetu dhidi ya wanyama hawa wakali na waharibifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nijibu maswali yake yote mawili kwa pamoja. Ninaomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri nitoe maelekezo kwa Kamishna Mkuu TAWA na TANAPA kwa kushirikiana na halmashahuri zetu kote nchini waende kuwaondoa wanyama hao ambao wapo katika makazi ya watu na katika mashamba yao. (Makofi)