Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Salum Khamis Salim
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bububu
Primary Question
MHE. SALUM K. SALIM aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa haraka na wa kudumu wa kuzuia tembo kuvamia Vijiji vya Meatu?
Supplementary Question 1
MHE. SALUM KHAMIS SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri, lakini kwa sababu suala la tembo katika Wilaya ya Meatu na Jimbo la Meatu limekuwa ni la siku nyingi na mkakati wake ni huu huu kila siku, na majibu ni hayo hayo, je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni kwamba, kuna sababu ya kuwa na azma kubwa ya kuwaondoa tembo ambao wanaishi maeneo ya watu kwa sasa? (Makofi)
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaomba kumpongeza sana Mheshimiwa Salum kwa kuwa na yeye sasa ni sehemu ya hifadhi na anashirikiana na taasisi zetu katika kuhami jamii yetu dhidi ya wanyama hawa wakali na waharibifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nijibu maswali yake yote mawili kwa pamoja. Ninaomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri nitoe maelekezo kwa Kamishna Mkuu TAWA na TANAPA kwa kushirikiana na halmashahuri zetu kote nchini waende kuwaondoa wanyama hao ambao wapo katika makazi ya watu na katika mashamba yao. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved