Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Ngonyani Msongozi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Daraja la Mtomoni?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, ninaomba nichukue nafasi hii kuishukuru sana Serikali kwa kuanza kujenga daraja lile ambalo lilikuwa linaleta athari kubwa kwa wananchi wa maeneo yale.

(a) Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba daraja hili linakamilika kwa wakati?

(b) Je, Naibu Waziri yupo tayari kuongozana nami kwenda katika eneo la ujenzi wa daraja hilo pale Mitomoni ili aweze kupokea zawadi kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri na kwa niaba ya Mheshimiwa Rais kwa sababu wananchi wamefurahi sana kuanzishwa kwa ujenzi wa Daraja?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan nipokee pongezi za Mheshimiwa Mbunge, ninaamini hizi ni pongezi pia za Wanaruvuma wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuhusu swali lake la (a), kwamba mikataba tuliyosaini na tulivyokubaliana na wenzetu wa World Bank, miradi yote hii inatakiwa ikamilishwe ndani ya mwaka mmoja na hatutegemei kuwa na changamoto yoyote ya mtiririko wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tulishakubaliana na wakandarasi, tunawasimamia tutahakikisha kwamba wanakamilisha hizo kazi kama tulivyokubaliana kwenye mkataba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kupokea zawadi kwa niaba ya Mheshimiwa Rais, ninataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakubaliana tarehe sahihi na tutakuwa tayari kwenda kupokea zawadi ya Wanaruvuma kwa ajili ya Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa ambayo ameifanya kujenga hili daraja muhimu sana, ahsante.