Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 6 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 60 2026-04-10

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha Wagonjwa wenye Ulemavu wa Akili wanapata Dawa bure kwa kuwa siyo wote wana Bima ya Afya?

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Sera ya Afya ya Mwaka 2007 inayoelekeza kutoa huduma za msamaha wa gharama za matibabu kwa watu wasio na uwezo na wenye magonjwa sugu kama saratani, UKIMWI, kisukari pamoja na wagonjwa ya akili.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshatangaza rasmi kuanza kwa utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote awamu ya kwanza, itakayohusisha makundi ya wananchi ikiwa ni pamoja na watoto, wajawazito, walemavu na wengine wasio na uwezo, ambapo kundi hili litagharamiwa na Serikali. Kukamilika kwa hatua hii kutawawezesha wananchi, wakiwemo walemavu wenye tatizo la afya ya akili kupata huduma pasipo kuwa na kikwazo cha fedha.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.