Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 10 | Other Sectors | Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi | 105 | 2026-04-16 |
Name
Dougras Didas Massaburi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kivule
Primary Question
MHE. DOUGRAS D. MASSABURI aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara ya Msongola – Mbande hadi Chamazi kwa kiwango cha lami?
Name
Abdallah Hamis Ulega
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkuranga
Answer
WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dougras Didas Massaburi, Mbunge wa Kivule, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Msongola – Mbande (kilometa 7.4) ni sehemu ya Barabara ya Chanika – Mbagala Rangitatu yenye jumla ya kilometa 29.2 ambapo jumla ya kilometa 25.4 zimejengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, ujenzi wa kilometa 3.8 zilizobaki katika sehemu ya Msongola – Mbande unaendelea ambapo kwa sasa jumla ya kilometa 1.6 zimewekwa tabaka la lami, kilometa 1.1 zipo kwenye tabaka la kokoto (CRR) na kilometa 1.1 zipo kwenye hatua za matabaka ya udongo. Ujenzi wa barabara hii unatarajia ukamilike mwezi Juni, 2026.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved