Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 99 2026-04-15

Name

Arif Suleiman Premji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ARIF S. PREMJI aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara kutoka Kijiji cha Hiyari kwenda Mkunwa - Makao Makuu ya Halmashauri kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Arifa Suleiman Premji, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Hiyari – Mkunwa kilometa 10 ni sehemu ya Barabara ya Mkoa ya kutoka Msijute – Mnima – Nanyamba yenye urefu wa kilometa 78.75, inayohudumiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS).

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inajengwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha, ambapo hadi sasa jumla ya kilometa mbili zimejengwa kwa kiwango cha lami kuanzia eneo la Msijute. Sehemu iliyobaki ya barabara hii itajengwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.