Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 26 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 333 | 2025-05-16 |
Name
Subira Khamis Mgalu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Bagamoyo
Primary Question
MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza:-
Je, lini Mradi wa Maji wa Mto Rufiji utaanza baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, ahsante, Serikali inaendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa mradi mkubwa wa kutoa maji Mto Rufiji ambao utanufaisha wakazi wa Mikoa ya Lindi, Pwani na Dar es Salaam. Usanifu huo unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka wa fedha 2024/2025 na Serikali itaanza kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved