Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 26 Water and Irrigation Wizara ya Maji 333 2025-05-16

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza:-

Je, lini Mradi wa Maji wa Mto Rufiji utaanza baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, Serikali inaendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa mradi mkubwa wa kutoa maji Mto Rufiji ambao utanufaisha wakazi wa Mikoa ya Lindi, Pwani na Dar es Salaam. Usanifu huo unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka wa fedha 2024/2025 na Serikali itaanza kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo. (Makofi)