Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 49 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 634 2025-06-19

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:-

Je, lini Kilimo cha Mazao ya Alizeti na chikichi kitaanza Mkoani Kagera kama alivyoagiza Mheshimiwa Rais akiwa Bukoba Juni, 2022?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika jitihada za kukuza kilimo cha mazao ya alizeti na chikichi katika Mkoa wa Kagera, Serikali kati ya mwaka 2021 na 2025 imesambaza jumla ya miche ya michikichi 15,840 katika Mkoa wa Kagera ili kuimarisha uzalishaji wa zao hilo. Pia, miche ya chikichi 2,908 inaendelea kutunzwa katika vitalu vya TARI - Maruku kwa ajili ya kusambazwa kwa wakulima wa zao la chikichi katika Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Serikali imehamasisha wakulima katika Mkoa wa Kagera kuongeza uzalishaji wa zao la alizeti kutoka tani 2,716.64 mwaka 2023 hadi tani 3,047 mwaka 2024, sawa na ongezeko la 12.16%.