Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 49 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 629 | 2025-06-19 |
Name
Michael Constantino Mwakamo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kibaha Vijijini
Primary Question
MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI K.n.y. MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: -
Je, zipi sababu za kuwa na gharama tofauti ya kuingiza Umeme majumbani Kibaha Vijijini badala ya kuwa na bei moja ya shilingi 27,000.00 tu?
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imetofautisha gharama za kuunganisha umeme kulingana na eneo husika ambapo kwa maeneo ya vijijini, gharama za kuunganisha umeme ni shilingi 27,000.00 na kwa maeneo ya mijini yakiwemo maeneo ya Miji Midogo gharama ni shilingi 320,960.00.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa eneo la Kibaha Vijijini, Kata za Kwala na Dutumi ni maeneo yanayopakana, vijijini hivyo vinalipa shilingi 27,000.00 kama gharama ya kuunganisha umeme. Aidha, maeneo yanayopatikana katika Kata za Mlandizi, Mtongani, Kawawa, Janga, Kikongo, Kilangalanga, Boko na Soga ni maeneo ya Mji Mdogo, hivyo wateja wa maeneo hayo wanalipia shilingi 320,960.00 kama gharama ya kuunganisha umeme.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved