Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 41 | Finance | Wizara ya Fedha | 528 | 2025-06-06 |
Name
Nusrat Shaaban Hanje
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -
Je, Serikali imepoteza fedha kiasi gani mwaka 2015 - 2020 kwa kutokuwepo usalama madhubuti wa mifumo ya usimamizi kufuatia mabadiliko ya TEHAMA? (Makofi)
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, mabadiliko ya TEHAMA yametumika kama fursa ya kujenga mifumo yetu wenyewe ya kukusanya mapato na kudhibiti matumizi. Mifumo hiyo imeiwezesha Serikali kukusanya mapato kwa ufanisi na hivyo kudhibiti kiwango cha uvujaji wa mapato kilichokuwepo kutokana na kutotumia mifumo ya kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato. Kwa mfano, mara baada ya kuanza kutumia mfumo wa kukusanya mapato wa GePG, mapato yasiyo ya kodi yanayokusanywa na Wizara, idara na taasisi yaliongezeka kutoka shilingi bilioni 689 mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi trilioni 2.21 mwaka 2019/2020 ikiwa ni ongezeko la takriban 400%.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved