Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 37 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo 481 2025-06-02

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuifanya lugha ya alama kuwa lugha rasmi ya mawasiliano?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua lugha ya alama kama mojawapo ya lugha rasmi za mawasiliano miongoni mwa wenzetu wenye changamoto ya usikivu hafifu. Aidha, Kanuni za Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) za mwaka 2019, Kifungu cha 34 (1 - 3) na 35 (1 - 3) vinaeleza namna bora ya usimamizi na uendeshaji wa ukalimani wa lugha ya alama ikiwa ni pamoja na kuunda kanzidata ya wakalimani wa lugha hiyo na kuratibu utumiaji wao katika shughuli mbalimbali za kiserikali na kijamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ni kusaidia ukuaji na weledi katika taaluma hii kwa kuwapatia mafunzo ya msasa yatakayowasaidia kuwa wakalimani bora na wanaoweza kutumiwa ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika, kupitia Kanuni hizo, tayari kanzidata ya wakalimani wa lugha hiyo imeanza kuundwa ambapo zaidi ya wakalimani 300 wamejisajili na hatua inayofuata ni kuwapa mafunzo na kubainisha wale wanaokidhi vigezo. Vilevile, muundo wa utumishi wa kada hii tayari umeandaliwa. Hatua nyingine zilizopangwa na Serikali ni pamoja na kuwawezesha wale watakaokidhi vigezo kujifunza pia alama za Kimataifa ili waweze kutumiwa ndani na nje ya nchi ya Tanzania.