Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 45 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 579 2025-06-12

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Bwawa la Lambo la kunyweshea mifugo Kijiji cha Kacheche na ujenzi wa Josho Nyikankulu, Kata ya Chala, Nkasi Kusini?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo la Nkasi Kusini, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, imejenga Bwawa la Kacheche kupitia Mpango wa Kuendeleza Kilimo (ASDP I) kati ya Mwaka 2008 na 2009. Hata hivyo kwa kuwa, bwawa hilo limejengwa muda mrefu, kwa sasa limejaa tope, na hivyo kupunguza uwezo wake wa kuhifadhi maji. Kutokana na hali hiyo, Serikali itatuma timu ya wataalam kufanya tathmini ya hali halisi ya bwawa hilo, ili hatua stahiki za kukamilisha ujenzi huo ziweze kuchukuliwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na ujenzi wa majosho katika maeneo mbalimbali hapa nchini, likiwemo Josho la Nyikankulu lililopo Kata ya Chala, Nkasi Kusini, kadiri ya upatikanaji wa fedha. Aidha, Naomba kutoa rai kwa Halmashauri ya Nkasi kutenga fedha kutoka kwenye mapato yake ya ndani, kwa ajili ya kujenga majosho katika maeneo yenye uhitaji wa huduma hiyo Wilayani Nkasi.