Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 33 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 428 2025-05-27

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma ya TEHAMA maeneo wanayotumia Wanafunzi kujisomea katika Vyuo Vikuu vya Umma?

Name

Omari Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inafanya maboresho ya Miundombinu ya Internet; Mifumo ya Kujifunzia Kidijitali (LMS); Maktaba za Kidijitali; Elimu kwa Studio za Multimedia; Mifumo ya Kiutawala Kidijiti na kununua Vifaa kwa Wanafunzi Wenye Mahitaji Maalum katika Vyuo Vikuu vya Umma. Lengo ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wa elimu ya juu wanapata mazingira bora ya kujisomea yanayochochea ujifunzaji wa kisasa, jumuishi, na unaotumia teknolojia kwa tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, mafanikio ya maboresho haya ni hatua muhimu katika mwelekeo wa kuifanya elimu ya juu nchini kuwa ya kisasa, jumuishi na yenye ushindani wa Kimataifa ili kufikia ajenda ya mageuzi ya elimu ya juu hapa nchini.