Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 32 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 402 | 2025-05-26 |
Name
Jonas William Mbunda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbinga Mjini
Primary Question
MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka Watumishi katika Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga ili kupunguza changamoto iliyopo?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutoa vibali vya ajira kila mwaka, ambapo kuanzia mwaka 2020/2021 hadi 2024/2025 jumla ya watumishi wa kada ya afya 34,720 wameajiriwa na kupangiwa vituo kote nchi. Katika kipindi cha mwaka 2020/2021 hadi 2024/2025 Halmashauri ya Mji wa Mbinga imepokea jumla ya watumishi 102 wa kada za afya na watumishi 36 wamepangiwa hospitali za wilaya na 66 katika vituo vya afya na zahanati.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa sekta ya afya kwa awamu na kuwapanga katika maeneo yenye upungufu wa wataalam, ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Mbinga.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved