Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 54 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 697 | 2025-06-26 |
Name
Kabula Enock Shitobela
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaongeza wataalam wa afya katika Hospitali ya Bugando na Sekou Toure kwa kuwa kuna upungufu mkubwa?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi Juni, 2025 Serikali imeajiri watumishi wapya 175 katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando na watumishi 79 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou Toure hivyo kuendelea kupunguza upungufu uliopo.
Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa kibali cha ajira za watumishi wa kada mbalimbali 144 kwa Hospitali ya Kanda Bugando ambapo taratibu za ajira zinaendelea.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved