Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 54 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 696 2025-06-26

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami barabara kutoka Mji Mdogo wa Laela – Mwimbi hadi Matai kuunganisha na Barabara ya Kasanga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Laela – Mwimbi – Kizombwe (Matai) yenye urefu wa kilometa 92 yameanza ambapo zabuni kwa ajili ya kumpata mhandisi mshauri wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na uandaaji wa nyaraka za zabuni ipo katika hatua ya kufanyiwa upekuzi (vetting).

Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zinatarajiwa kuchukua kipindi cha mwaka mmoja baada ya mkataba kusainiwa. Usanifu utakapokamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.