Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 54 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 695 | 2025-06-26 |
Name
Dr. Christina Christopher Mnzava
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuunganisha barabara kutoka Nyamilangano – Ushetu hadi Kaliua Tabora?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Barabara ya Nyamilangano – Ushetu – Kaliua ni sehemu ya barabara ya Mpanda – Ugalla – Kaliua – Ulyankulu – Kahama yenye urefu wa kilometa 457. Kazi ya upembuzi yakinifu (feasibility study) wa barabara hiyo imekamilika na mkataba wa kumpata mhandisi mshauri kwa ajili ya usanifu wa kina umewasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu kwa ajili ya upekuzi (vetting). Kazi ya usanifu wa kina itachukua muda wa miezi 12. Baada ya usanifu wa kina kukamilika Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved