Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 54 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 692 | 2025-06-26 |
Name
Jacquline Andrew Kainja
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: -
Je, lini TARURA itaweza kutengeneza barabara zenye viwango zisizoharibika kipindi cha mvua?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuimarisha uwezo wa kibajeti na rasilimali watu kwa TARURA ili kuwezesha ujenzi wa barabara za kudumu zenye viwango bora zaidi. Lengo ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma bora ya usafiri wakati wote wa mwaka na pia kuhakikisha barabara zinajengwa kwa viwango vinavyokidhi mahitaji ya kudumu na kwa kufuata usanifu wa kina uliofanyika huku ukizingatia viwango vya ubora vilivyowekwa, hususani katika kukabiliana na athari za hali ya hewa hasa katika nyakati za mvua.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, ni muhimu kufahamu kuwa barabara nyingi za vijijini bado ni za udongo na changarawe. Barabara hizi ni rahisi kuathiriwa na mvua nyingi na magari makubwa yanayozidi uwezo wake wa kubeba mizigo. Hali hii husababisha barabara hizi kuharibika haraka kuliko muda uliokusudiwa.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha mtandao wa barabara za vijijini na mijini kwa kuzijenga katika viwango vya kudumu kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved