Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 54 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 690 | 2025-06-26 |
Name
Mariamu Nassoro Kisangi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha majengo ya Mradi wa Dege Beach-NSSF Mbweni kwa kuwa ni wa muda mrefu?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya mradi wa Dege Eco Village uliopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam na kujiridhisha kuwa itakuwa ni hasara kuendelea na ujenzi wa mradi huo. Hivyo imeamriwa mradi huo uuzwe kwa wawekezaji wengine.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa mfuko unaendelea na hatua na taratibu za wawekezaji wenye nia ya kutwaa eneo hili kwa nia ya kununua mradi huo waweze kupewa.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved