Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 67 | 2025-04-14 |
Name
Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba kusini
Primary Question
MHE. OMARI M. KIGUA K.n.y MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha watumiaji wa Tanzania kununua bidhaa na huduma zinazozalishwa hapa nchini?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya bidhaa hizo kupitia mikakati mbalimbali ya ukuzaji biashara ndani na nje ya nchi. Mikakati hiyo ni pamoja na:-
(i) Kuanzishwa kwa rajamu/chapa maalum ya bidhaa ya Made in Tanzania ambayo itatumika kwa lengo la kutambulisha na kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini katika masoko yetu ya ndani na pia yale ya Kimataifa;
(ii) Kuratibu maonesho ya bidhaa za Tanzania (TIMEXPO) na Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayofanyika kila mwaka, ikiambatana na utekelezaji wa kampeni ya “Nunua bidhaa za Tanzania, Jenga uchumi wa Tanzania” ambapo wazalishaji, wasambazaji, wanunuzi pamoja na watoa huduma za usaidizi kutoka sekta za umma na binafsi hushiriki.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuhamasisha matumizi ya bidhaa zinazozalishwa nchini kupitia majukwaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na niliyoyataja hapo juu. Aidha, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kuwa mabalozi kwa kununua na kutumia bidhaa zinazozalishwa na wazalishaji wa ndani na kuhamasisha jamii ya Watanzania kuendelea kutumia bidhaa hizo. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved