Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 66 | 2025-04-14 |
Name
Hussein Nassor Amar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nyang'hwale
Primary Question
MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari la Zimamoto Wilaya ya Nyang’hwale?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji inatekeleza Mradi wa Ununuzi wa Magari na Vifaa vya Kuzimia Moto na Uokoaji wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 100 kutoka kampuni ya NAFFCO FZCO iliyopo Dubai. Mradi huo utawezesha kupatikana kwa vitendea kazi mbalimbali ikiwemo magari 150 ya kuzima moto na uokoaji yatakayosambazwa nchi nzima ikiwemo Wilaya ya Nyang’hwale.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali itaendelea kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kulipatia vitendea kazi ili liweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved