Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 63 | 2025-04-14 |
Name
Khadija Shaaban Taya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza:-
Je, Serikali imeweka utaratibu gani wa kuwasaidia matibabu ya ngozi watu wenye Ualbino kutokana na Ugonjwa wa Saratani ya Ngozi kuongezeka?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto wanazokabiliana nazo watu wenye ualbino. Serikali imechukua hatua kadhaa kusaidia matibabu na kinga ya saratani ya ngozi kwa watu wenye ualbino kwa kutekeleza yafuatayo:-
(i) Kuanzisha vituo maalum vya uchunguzi na matibabu ya saratani ya ngozi katika hospitali mbalimbali nchini ili kuhakikisha watu wenye ualbino wanapata huduma hizi kwa urahisi;
(ii) Kuimarisha upatikanaji na usambazaji wa vifaa kinga ikiwemo mafuta maalum ya kujikinga na jua ambayo yamejumuishwa kwenye bidhaa za afya zinazoagizwa na Bohari Kuu ya Dawa (MSD);
(iii) Serikali imeandaa Mpango Kazi wa Taifa wa Haki na Ustawi kwa Watu Wenye Ualbino, unaolenga kuboresha hali ya maisha ya watu wenye ualbino kwa kuimarisha huduma za afya, elimu na ulinzi dhidi ya saratani ya ngozi.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved