Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 62 | 2025-04-14 |
Name
Kabula Enock Shitobela
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA K. LUGANGIRA K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:-
Je, lini Serikali itatoa majibu ya tafiti zilizofanywa Kanda ya Ziwa kubaini visababishi vya kansa iliyokithiri?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya utafiti wa kina nchi nzima wa kusaidia kutambua kuwa ni saratani zipi zinaongoza katika Kanda ya Ziwa na kubaini kuwa saratani ya kibofu cha mkojo, saratani ya mji wa uzazi wa akinamama, saratani ya damu, macho na figo ndiyo zinazoongoza.
Mheshimiwa Spika, aidha, wataalam wamekusanya sampuli za damu 9600 za watu ambao hawana saratani ili kulinganisha na sampuli za damu za wenye saratani. Utafiti huu utasaidia kubaini chanzo cha hizo saratani. Hivyo kwa sasa bado utafiti unaendelea na visababishi vinavyosemwa bado ni nadharia tu kutokana na shughuli za kijamii katika maeneo husika.
Mheshimiwa Spika, hadi sasa mpango wa kudhibiti ongezeko umejikita katika kutoa elimu ya afya kwa viashiria vinavyodhaniwa pamoja na kuzingatia mkakati wa kitaifa wenye maeneo saba yaliyoainishwa ili kudhibiti viashiria vya saratani.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved