Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 61 | 2025-04-14 |
Name
Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Vwawa
Primary Question
MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:-
Je, lini Mradi wa Maji wa Ichenjezya, Hasamba, Nwansana, Vwawa hadi Ilolo utakamilika na kuanza kutoa maji ya uhakika?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Upanuzi wa Mtandao wa Maji Vwawa – Mlowo pamoja na Mradi wa Ukarabati wa Vyanzo vya maji Mwansyana na Mlowo. Utekelezaji wa Mradi huo wa Vwawa – Mlowo umefikia wastani wa 79% wakati Mradi wa Ukarabati wa Mwansyana – Mlowo umefikia wastani wa 94%. Tayari baadhi ya maeneo ya Mlowo Forest, Izyla, Saganoti, Malenje, Segerea, Mbimba, Ilolo Shule na Namleya yameanza kupata huduma ya maji kupitia miradi hiyo.
Mheshimiwa Spika, Miradi hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Mei, 2025 na kunufaisha wananchi wapatao 36,744 waishio kwenye Maeneo ya Hasamba, Ilolo, Vwawa, Ichenjezya, Mlowo Mabatini, Mlowo Mjini, Tazara, Kiwandani, Ichenjezya, Isangu, Hasanga, Mlowo Forest, Izyla, Saganoti, Malenje, Segerea, Mbimba, Ilolo Shule na Namleya.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved