Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 59 | 2025-04-14 |
Name
Khamis Yussuf Mussa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwahani
Primary Question
MHE. KHAMIS YUSSUF MUSSA aliuliza:-
Je, lini Serikali itainufaisha Zanzibar katika matumizi ya nishati ya gesi kutumika katika magari?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, mwezi Februari, 2022, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) iliingia makubaliano ya ushirikiano na Shirika la Maendeleo ya Petroli Zanzibar (ZPDC) ambapo kupitia ushirikiano huo masuala mbalimbali yamekuwa yakifanyika ikiwemo kubadilishana ujuzi na utaalam. Katika ushirikiano huu, suala la kupeleka gesi asilia Zanzibar ni mojawapo ya agenda kuu. Pande zote mbili bado zinaangalia namna bora ya kufikisha gesi asilia Zanzibar ili iweze kupatikana kwa bei rafiki kwa watumiaji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved