Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Finance and Planning | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 58 | 2025-04-14 |
Name
Minza Simon Mjika
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani kujenga miundombinu ya maji shuleni ili kuepuka milipuko ya magonjwa?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, shule 5,311 za Sekondari zina vyanzo vya maji vya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 2,960, visima shule 1,217 na wanaovuna maji ya mvua ni shule 1,134. Aidha, shule 20,509 za msingi zina vyanzo vya maji vya uhakika ambapo shule zenye maji ya bomba ni 10,965, visima shule 4,966 na shule zinazovuna maji ya mvua ni 4,578.
Mheshimiwa Spika, Mikakati ya Serikali ya kujenga miundombinu ya maji shuleni ili kuepuka milipuko ya magonjwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa: -
(a) Ujenzi wa shule mpya unajumuisha miundombinu ya maji inayohusisha kuvuna maji ya mvua, kuunganisha na mifumo ya Mamlaka za Maji na kuchimba visima;
(b) Ujenzi wa miundombinu ya vyoo unajumuisha wa miundombinu ya maji tiririka; na
(c) Kutumia sehemu ya fedha ya ruzuku ya uendeshaji wa shule kukarabati miundombinu ya maji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved