Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 57 | 2025-04-14 |
Name
Abdallah Dadi Chikota
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyamba
Primary Question
MHE. AGNES E. HOKORORO K.n.y. MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:-
Je, lini Serikali itatatua changamoto ya uhaba wa Walimu katika Halmashauri ya Mji Nanyamba?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa spika, Serikali inatambua changamoto ya uhaba ya walimu katika shule za Msingi na Sekondari nchini. Katika Mwaka wa Fedha 2024/2025, Serikali imeajiri walimu 15,925 ambapo walimu 27 na mafundi sanifu maabara wawili wamepangwa Halmashauri ya Mji Nanyamba. Serikali itaendelea kuajiri walimu na kuwapanga katika shule zenye upungufu katika Halmashauri ya Nanyamba. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved