Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 5 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 56 | 2025-04-14 |
Name
Sophia Hebron Mwakagenda
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-
Je, lini Serikali italitengeneza na kulitangaza Daraja la Mungu la kihistoria lililopo Wilaya ya Rungwe ambalo lipo katika hali ya kutotunzwa?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Daraja la Mungu lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe limetokana na mabadiliko asili ya miamba na kulifanya kuwa ni daraja ambalo halikuwahi kutengenezwa na mwanadamu hivyo kuwa kivutio cha utalii wa ndani na nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika, kutokana na sababu hiyo, daraja hili haliwezi kutengenezwa kwa njia za kibinadamu hivyo litaendelea kuwa la asili kama lilivyo kwani halitumiki kwa shughuli nyingine za kibinadamu isipokuwa kwa utalii pekee.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved