Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Dr. George Venance Lugomela (1 total)

MHE. DKT. GEORGE V. LUGOMELA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa tuna Kata ya Ipililo, kimejengwa kituo cha afya katika Kata ile na Kata ya Ipililo ndiyo Kata yenye wakazi wengi katika Jimbo la Maswa Mashariki. Ninaomba kuuliza, je, kituo cha afya hiki kitaanza kufanya kazi lini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge aliuliza swali la nyongeza kuhusu kituo cha afya Kata ya Maswa. Kwanza tumejielekeza kutoa katika vile vituo ambavyo havijakamilika kwanza viweze kutoa huduma zile za OPD. Kwa hiyo, mimi na Mheshimiwa Mbunge tutakaa chini baada ya Bunge hili leo, ili tuone namna gani katika kituo chetu hiki cha afya kitaanza kutoa huduma za msingi kwa ajili ya wananchi wetu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.