Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Cosmas Mtesigwa Bulala (1 total)

MHE. COSMAS M. BULALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Wizara ya TAMISEMI. Mji wa Ng’hungumalwa ni wa kibiashara katika Wilaya ya Kwimba. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa soko la kisasa katika kata hii na Mji wa Ng’hungumalwa, ambapo mwaka 2025 iliidhinishwa shilingi bilioni 3.9, kwa ajili ya kujenga stendi katika Mji wetu wa Ng’hungumalwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, miundombinu hiyo ni kipaumbele cha Serikali. Serikali inatambua uhitaji wa miundombinu hiyo, kwa hiyo, tutaendelea kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge na halmashauri kuhakikisha tunaanza kutenga fedha kwa awamu na kuhakikisha kwamba, tunajenga miundombinu hiyo.