Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Abdul Yussuf Maalim (1 total)

MHE. ABDUL YUSSUF MAALIM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nini mpango wa Serikali katika kutunza vyanzo vya maji, hasa vinavyopeleka maji katika Bwawa la Mwalimu Nyerere? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, upo mpango kabambe wa kutunza vyanzo vya maji vyote ambavyo vinapeleka maji katika Bwawa la Mwalimu Nyerere na vile ambavyo vinapeleka maji katika mabwawa, mito na maeneo mengine. Mpango wa kwanza ni kuhakikisha kwamba, tunawaambia wananchi wasimamie Mwongozo ule wa Mita 60 maana pale ndiyo kuna msingi wa uchafuzi na uharibifu wa vyanzo vya maji. Pale kuna wananchi wanalima, wanafanya shughuli za kilimo katika vyanzo vya maji, wengine wanafanya shughuli za viwanda katika vyanzo vya maji, wengine wanafuga katika vyanzo vya maji. Kwa hiyo, kwa kupitia mwongozo ule wa kusimamia sheria ya mita 60, tumekuwa tunaendelea kuwaelimisha wananchi sambamba na kuchukua hatua za kisheria kwa kuzingatia Sheria ya Mazingira. Nakushukuru. (Makofi)