Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Emmanuel John Khambay (1 total)

MHE. EMMANUEL J. KHAMBAY aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya maboresho ya makazi ya askari pamoja na kununua magari mapya Gereza la Babati Mjini?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Emmanuel John Khambay, Mbunge wa Babati Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Gereza la Babati ni miongoni mwa Magereza yaliyojengwa miaka mingi tangu mwaka 1974 hali iliyosababisha uchakavu wa miundombinu ya gereza pamoja na majengo ya makazi ya Askari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Magereza limeanza kutekeleza mpango mkakati wa muda mfupi na muda mrefu ambapo kwa Gereza Babati ziko nyumba tatu zinaendelea na ujenzi kwa kutumia mapato ya vyanzo vya ndani vya ubunifu. Aidha, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali imetenga shilingi 5,380,000,000/= kwa ajili ya ununuzi wa magari 31 kwa shughuli za Utawala na kusafirisha Mahabusu. Pindi magari hayo yatakapofika, Gereza la Babati litapatiwa gari moja mpya kwa matumizi ya kituo.