Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Jafari Wambura Chege (5 total)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026
MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipatia nafasi. Kwanza, nami nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatia nafasi ya kuchangia Wizara ya Ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili; kipekee kabisa nichukue nafasi kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mambo kadhaa, lakini nitataja matatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati ninaingia kwenye Bunge hili mara ya kwanza nilikuwa ni Mjumbe wa Kamati ya Maliasili na Utalii. Nje ya hivyo nimekuwa niki-declare interest mara zote ambazo ninachangia kwenye wizara hii kwamba, mimi ni mdau wa sekta ya ardhi, pia ndiyo professional yangu ambayo imenikuza kwa miaka yote.
Mheshimiwa Naibu Spika, mambo makubwa matatu ambayo yamekuwa yakizungumzwa kwenye taarifa zote za kamati na michango ya Bunge hili. Moja; tumekuwa tukizungumzia sana umuhimu wa Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995. La pili; tumekuwa tukizungumzia umuhimu wa RERA (Real Estate Regulatory Authority). Pia, tatu; tumekuwa tukizungumzia sana Kamisheni ya ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema nimeanza kutangulia kwa kipekee kabisa kuchukua nafasi kwa moyo wangu wa dhati kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa sababu haya yote matatu ambayo tumekuwa tukisema kwenye Bunge hili kwa miaka minne, kwenye Taarifa zetu za Kamati, kwenye michango ya Wabunge na ndiyo yamekuwa mapendekezo ya Kamati kwa miaka yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaona wakati huu wa Mheshimiwa Waziri Ndejembi, yametekelezwa na yamefanyika vizuri sana. Mheshimiwa Ndejembi hongera sana wewe pamoja na Naibu Waziri wako, watumishi wote wa Wizara kwa kweli wametufikisha vizuri sana. Hili si tu kwamba wamekosha Bunge lakini mmekidhi haja ya wadau wa sekta ya ardhi nchini. Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995, tumekuwa tukiisemea sana ifanyiwe mabadiliko ili iendane na kasi ya ukuaji wa uchumi na sekta ya ardhi nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995 tumekuwa tukiisemea sana ifanyiwe mabadiliko ili iendane na kasi ya ukuaji wa uchumi, iendane na kasi ya ukuaji wa Sekta ya Ardhi nchini, lakini maeneo mengine ilikuwa inamwacha mwanamke katika sekta ya umiliki wa ardhi hasa sehemu ya mirathi.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo kwenye Sera ya Taifa ya Ardhi tumeona inakwenda kumweka mwanamke kutambulika kumiliki ardhi, hata akinamama ambao wanakaa vijijini ambao kimsingi kwenye umiliki wa ardhi hasa maeneo ya mirathi walikuwa wameachwa, walikuwa hawana haki ya kumiliki ardhi, lakini sera hii inakwenda kutambua. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ninamwomba sana Mheshimiwa Waziri yale ambayo Mheshimiwa Rais ameyasema wakati anazindua sera hii, lakini pia malengo ambayo ameyaainisha kwenye taarifa yake na haya ambayo tumeyasema leo kupitia Bunge hili, nenda ukayafanye ili uweze kuboresha Sera hii ya Taifa ya Ardhi na iweze kufanya kazi vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ambalo ningetamani kwenye maeneo hayo ni kutambua mabadiliko ya kanuni na sheria mbalimbali kwenye sekta ya ardhi ambazo zinashabihiana na sekta ya ardhi nchini. Waziri anapofanya mabadiliko ya sera lazima aende akatambue sheria mbalimbali ambazo zinashabihiana na sekta ya ardhi nchini ili na zenyewe ziweze kufanyiwa mabadiliko ziendane na kasi yake na ziendane na dhamira na mwelekeo wa Mheshimiwa Rais nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema pia, lazima iendane na mabadiliko ya sheria na kanuni ya Wizara ya Ardhi peke yake. Kwa sababu zipo sheria, kama tunavyosema kwamba mwanamke sasa anakwenda kumiliki ardhi, tusipofanya mabadiliko ya Sheria ya Mirathi ya Ardhi maana yake itakuwa sera ipo, lakini mwanamke bado atakuwa hatambuliki katika umiliki wa sekta ya ardhi nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninamwomba pia Mheshimiwa Waziri tena katika sekta hii kwamba Mamlaka za Upangaji na Upimaji, sheria inasema hivyo, tunatambua sheria inasema kwamba, mwenye mamlaka ya upangaji na upimaji ni Mamlaka ya Serikali za Mitaa na mimi ni Mjumbe wa Kamati ya TAMISEMI. Ninamwomba sana Mheshimiwa Waziri, atengeneze connection kati ya Wizara ya TAMISEMI na Wizara yake kwa kutambua sera mama ili angalau sera hii iende ikatengeneze usimamizi mahiri, kwenye usimamizi kwa upande wa TAMISEMI, Wakurugenzi waweze kusimamia hili zoezi ambalo linatamkwa kwenye sheria lakini halifanyiki vile ambavyo inapaswa kufanyika kwa sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri lazima atambue kwamba mfumo wa usimamizi wa ardhi nchini siyo rafiki sana. Mfumo wa usimamizi wa ardhi nchini hauko rasmi kwa sababu hatuna chombo kinachosimamia Real Estate Regulatory Authority. Hatuna chombo kinachosimamia watu wa Real Estate Agent, hatuna chombo kinachosimamia Real Estate Developers Consultant, hawa brokers ambao wanafanya kazi zao. Nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kuja na RERA. Nimeona sasa wanakwenda kuunda hii taasisi, kuunda mfumo ambao utawaratibu na kuwasimamia hawa watu, hawa watu hawakuwa wanatambulika.

Mheshimiwa Naibu Spika, National Housing anafanya kazi ya usimamizi wa miliki, lakini zipo private company nyingi zinafanya kazi ya usimamizi wa miliki lakini hazitambuliki. Hazina Regulatory ambayo inawaongoza namna nzuri ya kwenda na kwa kutokuwa na usimamizi mahiri maana yake Serikali inakosa kodi, wao wanakuwa hawatambuliki na hata wao wanakosa wakati mwingine mikopo kwenye taasisi za Serikali kwa sababu hawaeleweki wako wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninamwomba Waziri hii RERA, Real Estate Regulatory Authority Mheshimiwa Waziri ipe kipaumbele sana kwa sababu watu wengi ambao ni brokers na Real Estate Agent wanakwama kwa sababu ya ukosefu wa kuwa na sheria ambayo inawasimamia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hili lipo jambo lingine ninaomba nimshauri Waziri. Ni kwenye mkopo wa KKK - kwenye Kupanga, Kupima na Kumilikisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kutoa fedha kwa miaka mingi mfululizo. Tumeona alitoa mara ya mwisho bilioni 50 kwenda kwenye Mamlaka za Upangaji na imetumika kwenye kupanga maeneo mengi nchini na kwenye Halmashauri. Ninamwomba tuzingatie mambo mawili. Pamoja na kuwa tumegundua kwamba kuna changamoto kubwa sana fedha hizi namna ya kurudi, baadhi ya Halmashauri hazirudishi fedha ipasavyo. Ninaomba mambo mawili haya angeyafanyia kazi ili angalau hizi fedha ziendelee kuwa na tija. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, wakati mikataba inasainiwa kati ya wakurugenzi na Wizara ya Ardhi, lazima TAMISEMI ihusike. Husisha TAMISEMI kama wasimamizi wa Wakurugenzi wale mnaosaini nao mikataba. Pili, anayetakiwa kuhusika, ni lazima umhusishe RAS wa Mkoa ili atambue na akusaidie namna ya kusimamia zile fedha zinazokwenda kwenye taasisi, kwenye maeneo ya Wakurugenzi. Haya mawili Mheshimiwa Waziri akiyafanya, itatusaidia sana kuhakikisha fedha hizi zinarudi kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima Wizara ya Fedha ihakikishe na yenyewe inahusika kwenye mkataba ule ili kurahisisha kusaidia zile fedha kurudi kwa wakati. Leo tunatoa bilioni 50, lakini Waziri mwenyewe anaona changamoto namna ya fedha hizi zinavyorudi, hii fedha ni revolving, inatakiwa irudi ili halmashauri zingine ziweze kupewa fedha, lakini hazirudi kwa wakati. Ninaomba sana Mheshimiwa Waziri hili alione na aone namna ambavyo wanaweza wakalifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine Mheshimiwa Waziri nimesema hapa ni Commission ya Ardhi Nchini. Kunakuwa hakuna connection kati ya Wizara ya Ardhi ambao ndiyo wanasimamia policy, TAMISEMI wanaosimamia sheria za utekelezaji wa ardhi, pamoja na watendaji wa maeneo yote mawili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Commission hii inakwenda sasa kuwa sehemu ya kusimamia yote mawili, inakwenda kusimamia utendaji wa Wizara ninyi wenyewe kwa yale yote wanayozungumza katika kupanga, kumilikisha ardhi, lakini pia inakwenda kuwa sehemu ya katikati kama broker au kuwarahisishia mahusiano yao wao na Wizara ya TAMISEMI. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maana yake ni nini? Kwanza itarahisisha upangaji na upimaji kwenda kwa kasi, itarahisisha master plan ambayo tumeizungumza ya sekta ya ardhi nchini itakwenda kwa kasi, pia itawasaidia kuondoa hilo gap ambalo mnalo kati ya sekta ya ardhi kwa maana ya Wizara ya Ardhi na TAMISEMI nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Waziri kuliona hili, kuanzisha Commission ya Ardhi, nimeona hapa anasema anaianzisha, hii iende kwa kasi kwa sababu kuna wakati hawakutani sekta ya ardhi na mipango au usimamizi wa sera na kule wasimamizi wa utekelezaji wanaotekeleza sheria, hawana namna ambavyo wanakutana ili kuhakikisha haya wanayafanya. Akiwa na Commission ya Ardhi itamsaidia sana Waziri angalau kufanya regulation na kuhakikisha kwamba haya mambo yote yanakwenda sawasawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine amelisema Mwenyekiti wa Kamati hii, juu ya utengano wa watumishi wa ardhi, hasa Maafisa Ardhi, Surveyors, Town Planners, hawa ambao wanaitika wako chini ya Kurugenzi, lakini wanaitika ndani ya Wizara. Huu mkanganyiko kwamba wako chini ya Mkurugenzi kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa, lakini wanawajibika kwenye sekta kwenye Wizara ya Ardhi nchini, kuna mkanganyiko mkubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema Mwenyekiti ni kwamba, wakati mwingine Wakurugenzi wanashindwa kuwatambua kama wako chini yao, kuna wakati mwingine wanapata maelekezo kutoka Wizara ya Ardhi juu ya jambo lolote linalotakiwa kufanywa kwenye sekta ya ardhi, hapo hapo anapata maelekezo kwa Mkurugenzi ambaye ndiyo bosi wake kwenye eneo lile la Mamlaka ya Serikali za Mitaa, ile contradiction inawafanya wale watu wanashindwa kuelewa wasimamie lipi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunamwomba sasa Mheshimiwa Waziri akae na Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI waamue hawa watumishi wakae upande upi. Ndiyo maana maeneo mengi hawa watu wanapata lawama kubwa sana, kwamba wanashindwa kutatua migogoro au wanashindwa ku-meet ile objective ambayo wamewapa ni kwa sababu ya hiyo contradiction, anapata maelekezo kwenye Wizara mbili tofauti, matokeo yake ni kwamba wanashindwa kusimamia na hawajui wasimamie lipi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba sana Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa hili Wakurugenzi wako chini ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa, wala hakuna sababu, wawarudishe kama walivyokuwa zamani, warudi kule chini ili wasimame kwenye command moja, ikitoka Wizara ya TAMISEMI inashuka mpaka kwa watumishi inakwenda, kuliko hivi ambavyo iko ilivyo hivi sasa. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa mud awa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa ni kengele ya pili.

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie jambo la mwisho kabisa ambalo ni kubwa ninatakiwa kulizungumza ni juu ya kupunguza gharama ya kumiliki ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona wamepunguza kiasi kikubwa sana cha fedha kwa wananchi wanaotaka kumiliki Hati ya Umiliki wa Ardhi nchini, ninamwomba sana hili Kamishna wa Ardhi atoke atoe semina kwa wananchi, ajue namna Mheshimiwa Rais alivyokubali na ameridhia kupunguza bei ya wananchi sasa kumiliki ardhi, zaidi ya asilimia kadhaa kwenye eneo hili ili angalau uweze kuongeza umiliki wa hati na ndiyo sehemu pekee inayoweza kutatua changamoto za ardhi nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana na naunga mkono hoja. Hongera sana kwa Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa nzuri, hongera sana Wizara ya Ardhi pamoja na watumishi wote. Ahsanteni sana. (Makofi)
Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/2027–2050/2051, Mapendekezo ya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2026/2027–2030/2031 na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2026/2027; na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali Katika Muda wa Kati ya 2026/2027 hadi 2028/2029.
MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa kutoka kwa Waziri Profesa Mkumbo, lakini pia nipate nafasi ya kuchangia mapendekezo ya mwongozo wa maandalizi ya bajeti kutoka kwa Waziri wa Fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kusema ninaunga mkono hoja zote mbili na ninakubaliana na maono yao mazuri yaliyopo kwenye taarifa zao zote mbili kwa Mawaziri hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuridhia na kukubali kuanzishwa mchakato wa Dira mpya ya Taifa ya mwaka 2050. Pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa mambo makuu matatu. Moja kwa kutekeleza maono ya Dkt. Samia, maono ya Watanzania na mwelekeo wao na dhamira waliyokuwa nayo juu ya kupatikana kwa dira mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili, nimpongeze pia Mheshimiwa Waziri kwa kuandaa mpango elekezi na dira yenyewe, kiukweli amefanya kazi kubwa nzuri kama ambavyo tunatambua changamoto ya Dira ya mwaka 2025 ilikwenda kwa kusuasua kwa sababu ya kukosekana kwa mpango elekezi wenyewe ya namna dira inavyokwenda kutekelezwa. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa hilo. La pili, nimpongeze pia kwenye taarifa yake kwa kutambua umuhimu wa wawekezaji hasa wazawa na kurudi kuangalia namna ambavyo Serikali inapaswa kushirikiana na private sectors bila kuwaacha wazawa katika kuinua uchumi wetu kama watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili Mheshimiwa Waziri aende alitazame upya pamoja na kwamba wazawa wanaruhusiwa kufanya kutekeleza miradi iliyo chini ya bilioni 50, ninashauri Serikali ipanue wigo iende zaidi ya bilioni 100 mpaka bilioni 200 kwa sababu ninaamini tunao wazawa ambao wana uwezo mkubwa wa kufanya haya. Tatu, nimpongeze Mheshimiwa Waziri, kwenye taarifa yake na ndiyo jambo muhimu sana la kuanza la kupendekeza walau Wakurugenzi wa Halmashauri kupata nafasi kulingana na uwezo wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hilo tu nimeona kwenye Kamati pia wamekwenda mbali wameshauri Wakurugenzi wa Taasisi mbalimbali na Mashirika ya Umma nao waende watazamwe katika nyanda hiyo, wateuliwe kulingana na nafasi zao ili tuweze kuwapima kulingana na ukuaji wa taasisi zao na utendaji wao wa moja kwa moja. Kwa hiyo, kwa kweli nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa taarifa hii. Nina maoni kadhaa kwa malengo mahususi katika dira. Yapo malengo mahususi manne, lakini nitajikita leo kwenye lengo moja tu la maisha bora na ustawi wake kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza dhana ya maisha bora, kama taifa linaloendelea tunatambua yapo maeneo kadhaa ambayo Serikali kwa ujumla wake inapaswa kujikita ili kuinua uchumi wa wananchi kwa ujumla wake. Wizara hii imeonesha mwelekeo na njia ya kupita, ni kazi sasa ya wizara za kisekta kuchukua maono ya wizara hii ya mipango na uwekezaji, kuyachakata na kuyaingiza kwenye mipango ya wizara za kisekta ili yaende yakashamiri na yasambae kwa wananchi kwenye maeneo yote kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye maeneo hayo nilitaka nijikite kwenye maeneo kadhaa. Mfano, tunapozungumzia maisha bora ni lazima uzungumze maisha bora kwa wananchi kwa kutazama miundombinu ya barabara inayozunguka wananchi wale. Katika miundombinu ya barabara lazima tuiangalie kwa nafasi mbili tofauti. Lazima tuangalie barabara zinazosimamiwa na TANROADS, lazima tuangalie barabara zinazosimamiwa na TARURA katika kutekeleza na kupunguza minong’ono na kuimarisha Maisha bora kwa ustawi wa wananchi wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utakubaliana na mimi, kuna baadhi ya meneo mengi sasa barabara imekuwa ni changamoto kubwa sana na Waheshimiwa Wabunge wamesema hapa, zipo barabara ambazo zimetangazwa, wakandarasi wapo site, wanatekeleza, zipo barabara ambazo zimesaini mikataba, wakandarasi hawajaingia site na zipo barabara ambazo zipo kwenye procurement process kwenye maeneo mbalimbali. Lazima tukubaliane kwa kuwa Wizara ya Fedha imesema hapa imetoa mwelekeo wake wa uandaaji wa bajeti, watenge fedha ya namna ya ukamilishaji wa barabara hizi kwenye maeneo yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko barabara ambazo tunazungumzia maisha bora kwa wananchi zimetajwa kwa awamu nne, tano kwenye maeneo tofauti toka miaka ya 95 zinatajwa barabara zile, mpaka sasa tuko mwaka 2025 tunakwenda 2030. Mfano wa Barabara yangu ya Utegi - Shirati kwenda Kirongwe ni matarajio yangu sasa Mheshimiwa Waziri, Wizara ya Fedha itatenga fedha kusaidia Wizara ya Ujenzi ili kuimarisha maisha bora kwenye maeneo yale, ili barabara zile ziweze kukamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara inapokamilika ndiyo inakwenda kuinua uchumi wa eneo husika kwa sababu kuna barabara zinaunganisha kati ya mkoa na mkoa, wilaya na wilaya na zingine zinaunganisha nchi na nchi. Kwa hiyo, katika kuimarisha na kutengeneza maisha bora lazima uweke fedha ya kukamilika kwa barabara ile ili wananchi waweze kupita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni utekelezaji wa miradi ya maji nchini. Niombe sana Wizara husika ya sekta ya maji, ifanye tathmini ijiridhishe badala ya kuwa na tathmini ya namna tumetatua maji kwa asilimia ngapi iangalie upatikanaji wa maji kwenye maeneo yale. Yako maeneo ambayo yana miundombinu ya maji, tunayahesabu kama asilimia katika kutekeleza mpango kazi wa maji, lakini maji hayatoki kwenye maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo wito wangu ni nini, Wizara ya Maji, kwanza ihakikishe miradi ya maji iliyoanzishwa inakamilika, inakwenda, inafika mwisho na inatoa maji. Mbili, wafanye tathmini kwenye miradi ambayo tayari walipeleka miundombinu badala ya kuihesabu kwenye asilimia ya utekelezaji wa maji wajiridhishe kama miradi hiyo kweli inatoa maji na wananchi wananufaika kwenye yale maeneo. Wakifanya hivyo, maana yake watakuwa wanakwenda kwenye ile itifaki ya maisha bora na ustawi wa wananchi kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu ni sekta ya ardhi, hili eneo tumekuwa tukilisahau sana. Kipanga, kupima na kumilikisha tumezungumza kwa mda mrefu sana. Niombe Waziri wa Sekta kwenye awamu hii ya bajeti inayokuja, hili jambo liende lipewe msukumo mkubwa kwa sababu ardhi isiyopangwa na kupimwa kwani ndiyo chanzo cha migogoro ya ardhi kwenye maeneo yetu, maana yake kunakuwa hakuna amani kwenye maeneo yetu. Ardhi yetu inakosa thamani halisi pale inapokuwa haijapangwa, kupimwa na kumilikishwa kwenye maeneo yao. Niombe sana Mheshimiwa Waziri husika, aende alione hili tunapokwenda kuchakata bajeti yake ili waweze kulipa nguvu ili waweze kupata ustawi ulio mzuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, limezungumzwa hapa jambo la soko la vijana, ajira kwa vijana na nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuanzisha Wizara husika ya Vijana, lakini ningeomba sana Waziri husika pamoja na michakato mbalimbali inayoendelea kwenye Wizara hii, lazima waende wakawa-group vijana, tujue hawa vijana wanaowazungumzia ni kuanzia umri upi mpaka umri gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, twende pia tukazungumze fursa sawa kwa hawa vijana kwa kutazama mazingira ya vijana wanayotoka. Kijana wa Rorya mazingira yake kwenye fursa hayawezi kuwa sana na kijana anayeishi Dar es Salaam. Kwa hiyo, Wizara iende ikajikite itazame kama inakwenda kusaidia vijana, isaidie vijana kulingana na mazingira ya maeneo yao wanayotoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, itazame fursa za kimaeneo hayo wanayotoka hao vijana. Tusizungumze general moja kwa moja kwa kuwa-generalize vijana wote kama vile ni sawa kutokana na fursa wanakotoka. Kijana wa Rorya inawezekana fursa yake isiwe sawa na kijana wa Tandahimba, haiwezi kuwa sawa na kijana wa Kinondoni. Kwa hiyo, ni lazima Mheshimiwa Waziri, aende alione hili namna ambavyo anaweza akaliweka ili litengeneze ustawi ulio mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwenye mpango, ni kuhusiana na kilimo. Sisi tunazungumza Mkoa wa Mara, leo hii hatuna zao kuu la kibiashara tunalojivunia, tunazo skim mbalimbali za umwagiliaji pamoja na kuzunguka Ziwa Victoria zaidi ya 70%, hatuna skim kubwa ya kuzungumza leo kama kielelezo cha ukuaji wa kilimo kwenye Mkoa wa Mara. Tunatamani Mheshimiwa Waziri wa Kilimo na mpango huu umekwishaonesha ili waende wakatengeneze upembuzi yakinifu kwenye maeneo yale na sisi tunatamani kupitia mkoa ule tuwe tuna skim ambazo zinawainua wananchi kwenye uchumi na zinaleta manufaa kwenye Wizara hii na kwenye sekta ya kilimo kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana Mheshimiwa Waziri alitazame hili. Mfano, mimi Rorya nimezungukwa na maji 77% lakini ninavyozungumza na wewe hatuna skim yoyote tunayojivunia pamoja na kuzungukwa na maji 77%. Tazama katika 100%, ni 23% peke yake nchi kavu, lakini sina skim yoyote ya umwagiliaji. Kwa hiyo, nikatamani pamoja na kusema, wenzangu wameshauri hapa kuwe na timu ya monitoring and evaluation lakini Wizara ione namna bora ya kusaidia maeneo haya ili waweze kuwasaidia kwenye kilimo, badala ya kubaki na kuzungumza kilimo kwa ujumla wake, lakini maeneo ambayo yana fursa hayanufaiki na kilimo hicho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ningetamani nizungumzie juu ya uchumi wa kimaeneo na Mheshimiwa Waziri amelizungumza sana hapa kwamba, pamoja na kwamba tunakwenda kuunda timu ya monitoring and evaluation lazima tuangalie maeneo hasa ya kimkoa namna yalivyokaa, ni fursa zipi za kiuchumi ambazo zinaweza zikaanzishwa zikawanufaisha mikoa husika. Mkoa wa Mara hatuna mradi mkubwa kama kielelezo kinavyozungumza, hatuna mradi wa skim ya umwagiliaji lakini viwanda tulivyokuwanavyo vyote vimekufa. Matarajio yetu ni nini kutoka kwa Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba, Serikali ione namna ambavyo kama fursa yetu ni kufufua viwanda vilivyokuwepo vikiwemo viwanda vya nguo, kiwanda cha maziwa na fursa zingine ambazo zinaweza zikainua uchumi wa maeneo yale. Ningetamani sana nione Wizara hii na Serikali ikiona namna ya kuweka fedha kuinua mkoa ule. Kwa sababu, ukifanya hivyo kwanza unainua ajira kwa wale vijana, lakini pia watatengeneza uchumi wa mkoa wenyewe husika, kuliko namna inavyokwenda kwa ujumla wake na sisi kama mkoa tunabaki tukiwa bado hatujapata kitu ambacho tunaweza tukasema tunajivunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi na ninasema tena kwa mara nyingine kwamba, ninaunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027
MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaanza kukushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi jioni ya leo kuwa mchangiaji wa kwanza katika Hotuba ya Waziri Mkuu pamoja na Taarifa za Kamati zilizo chini ya Wizara hii ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaanza kumpongeza na kumshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia kwa kazi kubwa nzuri ambayo ameendelea kufanya. Kwa muda wote ambao sisi kama Wabunge tumetoka kwenye maeneo yetu, tumeona mchango mkubwa kwenye maeneo yote na nyanja zote namna alivyowagusa wananchi wanyonge hasa kwenye maeneo mbalimbali ambayo ndiyo kimbilio lao kwenye maeneo mbalimbali kulingana na taarifa zilizosomwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili niendelee kumshukuru sana, ninachukua nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa nzuri, namna alivyoanza katika utendaji wake. Ziara alizofanya kwenye maeneo mengi ya nchi yetu zimeacha alama kwa namna ambavyo amekuwa akitatua changamoto za wananchi hawa wanyonge ambao sasa wanaamini kimbilio peke limekuwa yeye pamoja na Wizara yote kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, ninachukua nafasi kuwapongeza sana Waheshimiwa Mawaziri hasa Mawaziri wote walio chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu hususan Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Profesa Shemdoe, Naibu Mawaziri wawili pamoja na Makatibu Wakuu kwa kazi kubwa nzuri ambayo wameendelea kuifanya. Sisi kama Kamati tunajua mchango wao na namna walivyojitoa kuhudumia Wizara yetu hii ya TAMISEMI.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna msemo unasema: “Mwenye macho haambiwa tazama,” tulio wengi tuna macho na tunaona kazi kubwa nzuri inayofanywa na Serikali yetu chini ya jemedari Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye leo ameweka hotuba na bajeti yake kwenye Bunge hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo mambo kadhaa kama Mjumbe wa Kamati ya TAMISEMI na leo nitajikita kwenye eneo moja tu la Wizara ya TAMISEMI kama sehemu ya kutoa ushauri na kuboresha taarifa yetu ambayo Mheshimiwa Mwenyekiti wetu ametoka kuiwasilisha vizuri, ameisoma hapo mbele. Nitachangia mambo kadhaa katika mazingira ya kushauri na muktadha wa kushauri Serikali ili kuweza kuyaboresha.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza ni TARURA. Kwanza ninachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kama upande wa Serikali kuridhia fedha zote za Mfuko zilizokuwa zinakatwa kutoka kwenye tozo ya mafuta sasa kwenda moja kwa moja kwenye mifuko husika ili ziende zikatoe huduma TARURA. Hili ni jambo kubwa, ni jambo la kihistoria. Changamoto ya TARURA haikuwa fedha peke yake kuongezwa, pamoja na fedha kuongezwa, changamoto kubwa ya TARURA kutokufika kwenye maeneo mengi kutekeleza wajibu wao, ilikuwa ni pamoja na fedha kutokufika kwenye yale maeneo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa na fedha ilikuwa haifiki kwa sababu fedha nyingi tulikuwa tukikata kwenye tozo zilikuwa haziendi moja kwa moja katika kuhudumia barabara zetu kwenye maeneo yetu. Kwa maamuzi haya ya Serikali kama itaamua sasa fedha hizi zinazokatwa kutoka kwenye mafuta, moja kwa moja ziende kuhudumia TARURA, tunaamini kabisa TARURA sasa watakuwa na uwezo wa kujipambanua na kusimamia kufanya kazi kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kiukweli kwenye hili tunaipongeza sana Serikali kwa kuliona hili na ndilo lilikuwa ni wazo na maoni ya Kamati kuona kwamba fedha hizi kwa muda mrefu TARURA wamekuwa wakilia, fedha ilikuwa inakwenda kidogo ukilinganisha na mahitaji waliyokuwa nayo. Tuipongeze sana Serikali kwa kuliona hili, lakini pia tunapongeza Serikali kwa kuridhia sasa kuongeza bajeti ya TARURA, walikuwa wanapokea shilingi 944,000,000, sasa wanakwenda kupata fedha zaidi ya shilingi bilioni 1.2 katika utekelezaji wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ongezeko hili likienda sambamba na fedha hizi zinazokatwa kutoka kwenye tozo, kwenye miradi ya mafuta, ikienda huko tunaamini changamoto za barabara kwenye maeneo mengi itakuwa ni historia. Hili sisi kama Kamati tunalipongeza sana na tunajua ni kazi kubwa nzuri ambayo inafanywa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kutambua mchango mkubwa wa TARURA kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, liko jambo ambalo na sisi kama Kamati tumeliona. Pamoja na chanzo cha TARURA kuwa ni tozo, zipo halmashauri ambazo mwongozo wa TAMISEMI unasema, kama zinakusanya zaidi ya shilingi bilioni 10 na kuendelea, wanapaswa kupeleka 10% kuihudumia barabara zetu kwenye maeneo yetu. Sisi kama TAMISEMI, kama upande wa Kamati tumeona kwamba hili na lenyewe Wizara iisimamie Ofisi ya Waziri Mkuu kuhakikisha halmashauri na majiji yote yanayokusanya zaidi ya shilingi bilioni 10 na kuendelea wapeleke fedha hii 10% iende ikahudumie barabara za wananchi wetu kwenye maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni upande wa matundu ya vyoo. Kwanza ninampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuliona hili na kutoa miezi sita kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kulitekeleza, lakini jambo hili ni kubwa kuliko vile tunavyolitazama. Wakati wa mapitio ya bajeti, sisi kama TAMISEMI kwenye mikoa husika, tumegundua changamoto na upungufu wa matundu ya vyoo ni zaidi ya 100,000 mpaka 150,000 kwenye maeneo yote waliyokuwa wanaleta ile tathmini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nini ushauri wetu sisi kama Kamati, tukiziachia Mamlaka ya Serikali za Mitaa peke yake waende wakatatue changamoto ile, itachukua zaidi ya miaka mitano mpaka miaka sita kutatua changamoto ya kero kwenye maeneo yetu. Nami nichukue nafasi kuwapongeza viongozi kwa kuliona hili kwa sababu si jambo jema kuendelea kuzungumza matundu ya vyoo hasa kwenye Bunge hili. Ninakupongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kuliona hili na kutoa maelekezo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nini maoni yetu sisi juu ya hili; la kwanza, Wizara ya TAMISEMI ifanye tathmini ya kupitia sera ili waje na ratio ambayo inahitajika kwa wanafunzi 20 wanatumia matundu mangapi ya choo. Sasa hivi sera inasema wanafunzi 20 wanatumia tundu moja. Wanafunzi 20 kutumia tundu moja ukiweka kwenye shule ya wanafunzi zaidi ya 1,000, au 1,200 utahitaji matundu 50 mpaka 60 kuzunguka lile eneo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukaona sisi kama TAMISEMI kwamba vinginevyo kuna mahali itafika shule ukuta wake utazungukwa na matundu ya vyoo peke yake. Kwa hiyo tukasema, kwanza wapitie sera ile, waje na ratio ambayo inakwenda na dhana na uhalisia uliopo hivi sasa kwa sababu matundu haya wingi wa zaidi ya 100,000, 150,000 ni kwa sababu tunatumia ratio ambayo kimsingi inawezekana haiendi na uhalisia ulioko maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakifanya ile tathmini, wakapata uhalisia wa matundu mangapi yanatakiwa kwa mwanafunzi mmoja, then waje sasa Serikali itenge fedha na ninaamini watatekeleza kwa muda kwa namna ambayo litatakiwa lifanyike.

Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, tulijadili juu ya NeST kwa maana ya bakaa. Hili jambo ni jambo mtambuka. Kwanza mimi binafsi ni miongoni mwa Wabaunge wachache ambao hawaamini kwamba NeST inatakiwa ifutwe turudi kule tulikotoka. Kama Waheshimiwa Wabunge wanakumbuka, wakati ule Afisa Manunuzi mmoja alikuwa anaamua nani ampe mradi na anatanguliza za kwake juu, anatoa, bila usimamizi wowote wa miradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, NeST inazo changamoto zake ambazo zingine ziko ndani ya uwezo wa Serikali wanapaswa kuzitatua. La kwanza, lazima PPRA waendelee kutoa elimu namna ya kutumia Mfumo wa NeST kwenye maeneo yote, kwenye halmashauri zote. La pili, Serikali lazima ipeleke fedha za miradi ya maendeleo zinazopotakiwa kupelekwa kabla ya muda haujafika mwisho wa mwaka wa bajeti. Kwa mfano, leo tutanazungumza mwezi Aprili, fedha za miradi ya maendeleo kwenye halmashauri nyingine bado hazijaenda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunawapelekea halmashauri fedha, mwezi wa sita tunafunga mwaka (tunakwenda kumaliza ule mwaka) na tunataka wazitumie kabla ya tarehe 31 Juni, wataitumiaje hii fedha? Kwa hiyo, utakuta kwamba tunamaliza mwaka wakati wanakwenda kutangaza kunakuwa na mrundikano wa maombi kwenye Mfumo wa NeST na kunapokuwa na mrundikano wa maombi kwenye Mfumo wa NeST, tunajikuta tunavuka na ile fedha kwenda kwenye mwaka mwingine wa bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, kurundikana kwa fedha hizi mwishoni kwenye hatima yake tunagundua kwamba NeST, watu wengine wanaweza wakasema NeST haifanyi kazi. Ni kweli ninakiri kwamba wapo watu ambao wamejificha kwenye kivuli cha NeST, wanashindwa kusimamia majukumu yao, wanashindwa kutenda kazi. Sasa malengo yao ni kuhakikisha ule Mfumo unafutwa turudi tulikotoka kule nyuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Wabunge lazima tuiombe Serikali iboreshe namna ya matumizi bora ya Mfumo wa NeST, lazima wasimamie fedha za miradi ya maendeleo ziende kwa muda ndani ya quarter ya tatu fedha ziwe zimekwenda. Kuanzia mwezi Desemba, hadi mwezi Januari, fedha za miradi ya maendeleo zianze kwenda, halmashauri zitangaze kazi ili tuwe na muda wa kufanya assessment ya kujiridhisha akina nani wanaomba na tuweze kuisimamia vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, lipo suala lingine la migogoro ya ardhi ambalo kwenye hotuba yake Mheshimiwa Waziri Mkuu ameligusa. Lazima tukubaliane hapa, pamoja na kwamba hati ni zao la mwisho la umiliki wa ardhi kwa mwananchi yeyote, lazima kuna hatua kadhaa zinazopitiwa. La kwanza, lazima uwe na PP lazima eneo lile lipangwe matumizi bora ya ardhi. La pili, lazima eneo lile lipimwe. Ukipima ukipata survey plan ndiyo unakwenda hatua ya tatu ya umilikaji wa kupewa hati.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengi, lazima tu-plan na Waziri wa Ardhi alichukue hili. Mfumo wetu wa utoaji wa hati, mfumo wetu wa TEHAMA ambao unasimamia mlolongo mzima wa utoaji wa hati mpaka sasa una changamoto nyingi sana. Leo Mbunge ukienda pale unaenda kuomba hati Dodoma, utakaa zaidi ya siku moja, siku mbili, shida ni mfumo huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kabla ya kwenda kwenye hatima yetu ya mwisho, ninashauri sana Mheshimiwa Waziri afanye mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, apitie mfumo wenyewe, mfumo wa TEHAMA wa utoaji na usimamizi wa utoaji wa hati, wenyewe kwanza. Uwe na uwezo wa ku-generate Town Planning yenyewe, iwe na uwezo wa ku-generate TP yenyewe na uwe na uwezo wa kutoa hati bila kuingiliwa na mtu yeyote na utoe kwa uharaka ili angalau hizi changamoto zisiwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni kuhakikisha kwamba ardhi maeneo yote inapangwa na kupimwa. Changamoto katika kijiji na kijiji kwa sababu maeneo mengi hakuna mipaka kati ya kijiji na kijiji, hazijapangwa na kupimwa. Ile collision ya wananchi kwamba kijiji kingine na kijiji kingine wakiingiliana wanazalisha mgomo kwenye maeneo yetu. Tunamwomba sana Mheshimiwa Waziri alione hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa Serikali ni kuwekeza fedha kuhakikisha maeneo yote yanapangwa kwa matumizi sahihi ili kupunguza changamoto zilizoko kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, kwa harakaharaka nitakwenda kumalizia, ni 10% ya mikopo ya vijana. Hapa tumegundua changamoto kubwa sana sisi kama Kamati. Leo hii ukichukua halmashauri kwa maana ya manispaa zilizo Mkoa wa Dar es Salaam peke yake fedha ambazo wameweka benki 10%, waliyokata hapa ni mapato wanayokusanya, 10% wakaweka benki, siyo chini ya zaidi ya shilingi bilioni 60 kwenye Halmashauri za Dar es Salaam peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumefanya tathmini halmashauri zote nchini 186, zaidi ya shilingi bilioni 100 na kitu zipo benki zinasubiri vijana waende wakakope. Changamoto tuliyoiona ni kwamba, kwanza ni upungufu wa vijana; elimu haijatoka vizuri ya kuwahamasisha kwenda kukopa, hilo la kwanza, lakini Maafisa Maendeleo ya Jamii hawajajitoa kuona hii fursa pekee ya kutoa elimu, ili vijana waende wakakope.

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika ni fedha ile sasa imekaa benki, fedha nyingi ambayo imerundikana kule ndani, ninashauri, lazima Serikali itazame. Tunachoogopa ni fedha ile ikikaa zaidi ya miaka mitatu/minne anayefaidika ni benki hizi za kibiashara, sisi kama Serikali hakuna mtu atafaidika kwa sababu, wao wana-earn interest kutokana na ile fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati fedha ile inakwenda kukaa benki unakuta halmashauri hizo hawana chai, hawana madawati, hawana zahanati, lakini wamechukua mabilioni ya fedha yamewekwa, wanasubiri vijana wakope. Ninaishauri Wizara, Mheshimiwa Waziri Mkuu na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, wafanye-assessment ya kujiridhisha kama kuna uwezokano wa kufanya mabadiliko ya mwongozo na kanuni, ili fedha hizo wakati mwingine zikizidi ziende zikatumike kwenye mahitaji muhimu yanayowagusa wananchi wa maeneo yale badala ya kubaki kurundikana benki. Kimsingi, mwisho wake hatujui ni upi kwa sababu, fedha zimekaa kule na hatujajua mwongozo wake mwishoni unasema nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunipa nafasi niwe mchangiaji wa kwanza jioni ya leo. Ninaunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027
MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaanza kukushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi jioni ya leo kuwa mchangiaji wa kwanza katika Hotuba ya Waziri Mkuu pamoja na Taarifa za Kamati zilizo chini ya Wizara hii ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaanza kumpongeza na kumshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia kwa kazi kubwa nzuri ambayo ameendelea kufanya. Kwa muda wote ambao sisi kama Wabunge tumetoka kwenye maeneo yetu, tumeona mchango mkubwa kwenye maeneo yote na nyanja zote namna alivyowagusa wananchi wanyonge hasa kwenye maeneo mbalimbali ambayo ndiyo kimbilio lao kwenye maeneo mbalimbali kulingana na taarifa zilizosomwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili niendelee kumshukuru sana, ninachukua nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa nzuri, namna alivyoanza katika utendaji wake. Ziara alizofanya kwenye maeneo mengi ya nchi yetu zimeacha alama kwa namna ambavyo amekuwa akitatua changamoto za wananchi hawa wanyonge ambao sasa wanaamini kimbilio peke limekuwa yeye pamoja na Wizara yote kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, ninachukua nafasi kuwapongeza sana Waheshimiwa Mawaziri hasa Mawaziri wote walio chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu hususan Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Profesa Shemdoe, Naibu Mawaziri wawili pamoja na Makatibu Wakuu kwa kazi kubwa nzuri ambayo wameendelea kuifanya. Sisi kama Kamati tunajua mchango wao na namna walivyojitoa kuhudumia Wizara yetu hii ya TAMISEMI.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna msemo unasema: “Mwenye macho haambiwa tazama,” tulio wengi tuna macho na tunaona kazi kubwa nzuri inayofanywa na Serikali yetu chini ya jemedari Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye leo ameweka hotuba na bajeti yake kwenye Bunge hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo mambo kadhaa kama Mjumbe wa Kamati ya TAMISEMI na leo nitajikita kwenye eneo moja tu la Wizara ya TAMISEMI kama sehemu ya kutoa ushauri na kuboresha taarifa yetu ambayo Mheshimiwa Mwenyekiti wetu ametoka kuiwasilisha vizuri, ameisoma hapo mbele. Nitachangia mambo kadhaa katika mazingira ya kushauri na muktadha wa kushauri Serikali ili kuweza kuyaboresha.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza ni TARURA. Kwanza ninachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kama upande wa Serikali kuridhia fedha zote za Mfuko zilizokuwa zinakatwa kutoka kwenye tozo ya mafuta sasa kwenda moja kwa moja kwenye mifuko husika ili ziende zikatoe huduma TARURA. Hili ni jambo kubwa, ni jambo la kihistoria. Changamoto ya TARURA haikuwa fedha peke yake kuongezwa, pamoja na fedha kuongezwa, changamoto kubwa ya TARURA kutokufika kwenye maeneo mengi kutekeleza wajibu wao, ilikuwa ni pamoja na fedha kutokufika kwenye yale maeneo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa na fedha ilikuwa haifiki kwa sababu fedha nyingi tulikuwa tukikata kwenye tozo zilikuwa haziendi moja kwa moja katika kuhudumia barabara zetu kwenye maeneo yetu. Kwa maamuzi haya ya Serikali kama itaamua sasa fedha hizi zinazokatwa kutoka kwenye mafuta, moja kwa moja ziende kuhudumia TARURA, tunaamini kabisa TARURA sasa watakuwa na uwezo wa kujipambanua na kusimamia kufanya kazi kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kiukweli kwenye hili tunaipongeza sana Serikali kwa kuliona hili na ndilo lilikuwa ni wazo na maoni ya Kamati kuona kwamba fedha hizi kwa muda mrefu TARURA wamekuwa wakilia, fedha ilikuwa inakwenda kidogo ukilinganisha na mahitaji waliyokuwa nayo. Tuipongeze sana Serikali kwa kuliona hili, lakini pia tunapongeza Serikali kwa kuridhia sasa kuongeza bajeti ya TARURA, walikuwa wanapokea shilingi 944,000,000, sasa wanakwenda kupata fedha zaidi ya shilingi bilioni 1.2 katika utekelezaji wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ongezeko hili likienda sambamba na fedha hizi zinazokatwa kutoka kwenye tozo, kwenye miradi ya mafuta, ikienda huko tunaamini changamoto za barabara kwenye maeneo mengi itakuwa ni historia. Hili sisi kama Kamati tunalipongeza sana na tunajua ni kazi kubwa nzuri ambayo inafanywa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kutambua mchango mkubwa wa TARURA kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, liko jambo ambalo na sisi kama Kamati tumeliona. Pamoja na chanzo cha TARURA kuwa ni tozo, zipo halmashauri ambazo mwongozo wa TAMISEMI unasema, kama zinakusanya zaidi ya shilingi bilioni 10 na kuendelea, wanapaswa kupeleka 10% kuihudumia barabara zetu kwenye maeneo yetu. Sisi kama TAMISEMI, kama upande wa Kamati tumeona kwamba hili na lenyewe Wizara iisimamie Ofisi ya Waziri Mkuu kuhakikisha halmashauri na majiji yote yanayokusanya zaidi ya shilingi bilioni 10 na kuendelea wapeleke fedha hii 10% iende ikahudumie barabara za wananchi wetu kwenye maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni upande wa matundu ya vyoo. Kwanza ninampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuliona hili na kutoa miezi sita kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kulitekeleza, lakini jambo hili ni kubwa kuliko vile tunavyolitazama. Wakati wa mapitio ya bajeti, sisi kama TAMISEMI kwenye mikoa husika, tumegundua changamoto na upungufu wa matundu ya vyoo ni zaidi ya 100,000 mpaka 150,000 kwenye maeneo yote waliyokuwa wanaleta ile tathmini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nini ushauri wetu sisi kama Kamati, tukiziachia Mamlaka ya Serikali za Mitaa peke yake waende wakatatue changamoto ile, itachukua zaidi ya miaka mitano mpaka miaka sita kutatua changamoto ya kero kwenye maeneo yetu. Nami nichukue nafasi kuwapongeza viongozi kwa kuliona hili kwa sababu si jambo jema kuendelea kuzungumza matundu ya vyoo hasa kwenye Bunge hili. Ninakupongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kuliona hili na kutoa maelekezo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nini maoni yetu sisi juu ya hili; la kwanza, Wizara ya TAMISEMI ifanye tathmini ya kupitia sera ili waje na ratio ambayo inahitajika kwa wanafunzi 20 wanatumia matundu mangapi ya choo. Sasa hivi sera inasema wanafunzi 20 wanatumia tundu moja. Wanafunzi 20 kutumia tundu moja ukiweka kwenye shule ya wanafunzi zaidi ya 1,000, au 1,200 utahitaji matundu 50 mpaka 60 kuzunguka lile eneo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukaona sisi kama TAMISEMI kwamba vinginevyo kuna mahali itafika shule ukuta wake utazungukwa na matundu ya vyoo peke yake. Kwa hiyo tukasema, kwanza wapitie sera ile, waje na ratio ambayo inakwenda na dhana na uhalisia uliopo hivi sasa kwa sababu matundu haya wingi wa zaidi ya 100,000, 150,000 ni kwa sababu tunatumia ratio ambayo kimsingi inawezekana haiendi na uhalisia ulioko maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakifanya ile tathmini, wakapata uhalisia wa matundu mangapi yanatakiwa kwa mwanafunzi mmoja, then waje sasa Serikali itenge fedha na ninaamini watatekeleza kwa muda kwa namna ambayo litatakiwa lifanyike.

Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, tulijadili juu ya NeST kwa maana ya bakaa. Hili jambo ni jambo mtambuka. Kwanza mimi binafsi ni miongoni mwa Wabaunge wachache ambao hawaamini kwamba NeST inatakiwa ifutwe turudi kule tulikotoka. Kama Waheshimiwa Wabunge wanakumbuka, wakati ule Afisa Manunuzi mmoja alikuwa anaamua nani ampe mradi na anatanguliza za kwake juu, anatoa, bila usimamizi wowote wa miradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, NeST inazo changamoto zake ambazo zingine ziko ndani ya uwezo wa Serikali wanapaswa kuzitatua. La kwanza, lazima PPRA waendelee kutoa elimu namna ya kutumia Mfumo wa NeST kwenye maeneo yote, kwenye halmashauri zote. La pili, Serikali lazima ipeleke fedha za miradi ya maendeleo zinazopotakiwa kupelekwa kabla ya muda haujafika mwisho wa mwaka wa bajeti. Kwa mfano, leo tutanazungumza mwezi Aprili, fedha za miradi ya maendeleo kwenye halmashauri nyingine bado hazijaenda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunawapelekea halmashauri fedha, mwezi wa sita tunafunga mwaka (tunakwenda kumaliza ule mwaka) na tunataka wazitumie kabla ya tarehe 31 Juni, wataitumiaje hii fedha? Kwa hiyo, utakuta kwamba tunamaliza mwaka wakati wanakwenda kutangaza kunakuwa na mrundikano wa maombi kwenye Mfumo wa NeST na kunapokuwa na mrundikano wa maombi kwenye Mfumo wa NeST, tunajikuta tunavuka na ile fedha kwenda kwenye mwaka mwingine wa bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, kurundikana kwa fedha hizi mwishoni kwenye hatima yake tunagundua kwamba NeST, watu wengine wanaweza wakasema NeST haifanyi kazi. Ni kweli ninakiri kwamba wapo watu ambao wamejificha kwenye kivuli cha NeST, wanashindwa kusimamia majukumu yao, wanashindwa kutenda kazi. Sasa malengo yao ni kuhakikisha ule Mfumo unafutwa turudi tulikotoka kule nyuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Wabunge lazima tuiombe Serikali iboreshe namna ya matumizi bora ya Mfumo wa NeST, lazima wasimamie fedha za miradi ya maendeleo ziende kwa muda ndani ya quarter ya tatu fedha ziwe zimekwenda. Kuanzia mwezi Desemba, hadi mwezi Januari, fedha za miradi ya maendeleo zianze kwenda, halmashauri zitangaze kazi ili tuwe na muda wa kufanya assessment ya kujiridhisha akina nani wanaomba na tuweze kuisimamia vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, lipo suala lingine la migogoro ya ardhi ambalo kwenye hotuba yake Mheshimiwa Waziri Mkuu ameligusa. Lazima tukubaliane hapa, pamoja na kwamba hati ni zao la mwisho la umiliki wa ardhi kwa mwananchi yeyote, lazima kuna hatua kadhaa zinazopitiwa. La kwanza, lazima uwe na PP lazima eneo lile lipangwe matumizi bora ya ardhi. La pili, lazima eneo lile lipimwe. Ukipima ukipata survey plan ndiyo unakwenda hatua ya tatu ya umilikaji wa kupewa hati.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengi, lazima tu-plan na Waziri wa Ardhi alichukue hili. Mfumo wetu wa utoaji wa hati, mfumo wetu wa TEHAMA ambao unasimamia mlolongo mzima wa utoaji wa hati mpaka sasa una changamoto nyingi sana. Leo Mbunge ukienda pale unaenda kuomba hati Dodoma, utakaa zaidi ya siku moja, siku mbili, shida ni mfumo huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kabla ya kwenda kwenye hatima yetu ya mwisho, ninashauri sana Mheshimiwa Waziri afanye mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, apitie mfumo wenyewe, mfumo wa TEHAMA wa utoaji na usimamizi wa utoaji wa hati, wenyewe kwanza. Uwe na uwezo wa ku-generate Town Planning yenyewe, iwe na uwezo wa ku-generate TP yenyewe na uwe na uwezo wa kutoa hati bila kuingiliwa na mtu yeyote na utoe kwa uharaka ili angalau hizi changamoto zisiwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni kuhakikisha kwamba ardhi maeneo yote inapangwa na kupimwa. Changamoto katika kijiji na kijiji kwa sababu maeneo mengi hakuna mipaka kati ya kijiji na kijiji, hazijapangwa na kupimwa. Ile collision ya wananchi kwamba kijiji kingine na kijiji kingine wakiingiliana wanazalisha mgomo kwenye maeneo yetu. Tunamwomba sana Mheshimiwa Waziri alione hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa Serikali ni kuwekeza fedha kuhakikisha maeneo yote yanapangwa kwa matumizi sahihi ili kupunguza changamoto zilizoko kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, kwa harakaharaka nitakwenda kumalizia, ni 10% ya mikopo ya vijana. Hapa tumegundua changamoto kubwa sana sisi kama Kamati. Leo hii ukichukua halmashauri kwa maana ya manispaa zilizo Mkoa wa Dar es Salaam peke yake fedha ambazo wameweka benki 10%, waliyokata hapa ni mapato wanayokusanya, 10% wakaweka benki, siyo chini ya zaidi ya shilingi bilioni 60 kwenye Halmashauri za Dar es Salaam peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumefanya tathmini halmashauri zote nchini 186, zaidi ya shilingi bilioni 100 na kitu zipo benki zinasubiri vijana waende wakakope. Changamoto tuliyoiona ni kwamba, kwanza ni upungufu wa vijana; elimu haijatoka vizuri ya kuwahamasisha kwenda kukopa, hilo la kwanza, lakini Maafisa Maendeleo ya Jamii hawajajitoa kuona hii fursa pekee ya kutoa elimu, ili vijana waende wakakope.

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika ni fedha ile sasa imekaa benki, fedha nyingi ambayo imerundikana kule ndani, ninashauri, lazima Serikali itazame. Tunachoogopa ni fedha ile ikikaa zaidi ya miaka mitatu/minne anayefaidika ni benki hizi za kibiashara, sisi kama Serikali hakuna mtu atafaidika kwa sababu, wao wana-earn interest kutokana na ile fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati fedha ile inakwenda kukaa benki unakuta halmashauri hizo hawana chai, hawana madawati, hawana zahanati, lakini wamechukua mabilioni ya fedha yamewekwa, wanasubiri vijana wakope. Ninaishauri Wizara, Mheshimiwa Waziri Mkuu na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, wafanye-assessment ya kujiridhisha kama kuna uwezokano wa kufanya mabadiliko ya mwongozo na kanuni, ili fedha hizo wakati mwingine zikizidi ziende zikatumike kwenye mahitaji muhimu yanayowagusa wananchi wa maeneo yale badala ya kubaki kurundikana benki. Kimsingi, mwisho wake hatujui ni upi kwa sababu, fedha zimekaa kule na hatujajua mwongozo wake mwishoni unasema nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunipa nafasi niwe mchangiaji wa kwanza jioni ya leo. Ninaunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)

Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda mrefu 2026/2027 - 2050/2051, Mapendekezo ya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/2027 – 2030/2031) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2026/2027 na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali katika Muda wa Kati ya 2026/2027 - 2028/2029
MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa kutoka kwa Waziri Profesa Mkumbo, lakini pia nipate nafasi ya kuchangia mapendekezo ya mwongozo wa maandalizi ya bajeti kutoka kwa Waziri wa Fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kusema ninaunga mkono hoja zote mbili na ninakubaliana na maono yao mazuri yaliyopo kwenye taarifa zao zote mbili kwa Mawaziri hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuridhia na kukubali kuanzishwa mchakato wa Dira mpya ya Taifa ya mwaka 2050. Pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa mambo makuu matatu. Moja kwa kutekeleza maono ya Dkt. Samia, maono ya Watanzania na mwelekeo wao na dhamira waliyokuwa nayo juu ya kupatikana kwa dira mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili, nimpongeze pia Mheshimiwa Waziri kwa kuandaa mpango elekezi na dira yenyewe, kiukweli amefanya kazi kubwa nzuri kama ambavyo tunatambua changamoto ya Dira ya mwaka 2025 ilikwenda kwa kusuasua kwa sababu ya kukosekana kwa mpango elekezi wenyewe ya namna dira inavyokwenda kutekelezwa. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa hilo. La pili, nimpongeze pia kwenye taarifa yake kwa kutambua umuhimu wa wawekezaji hasa wazawa na kurudi kuangalia namna ambavyo Serikali inapaswa kushirikiana na private sectors bila kuwaacha wazawa katika kuinua uchumi wetu kama watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili Mheshimiwa Waziri aende alitazame upya pamoja na kwamba wazawa wanaruhusiwa kufanya kutekeleza miradi iliyo chini ya bilioni 50, ninashauri Serikali ipanue wigo iende zaidi ya bilioni 100 mpaka bilioni 200 kwa sababu ninaamini tunao wazawa ambao wana uwezo mkubwa wa kufanya haya. Tatu, nimpongeze Mheshimiwa Waziri, kwenye taarifa yake na ndiyo jambo muhimu sana la kuanza la kupendekeza walau Wakurugenzi wa Halmashauri kupata nafasi kulingana na uwezo wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hilo tu nimeona kwenye Kamati pia wamekwenda mbali wameshauri Wakurugenzi wa Taasisi mbalimbali na Mashirika ya Umma nao waende watazamwe katika nyanda hiyo, wateuliwe kulingana na nafasi zao ili tuweze kuwapima kulingana na ukuaji wa taasisi zao na utendaji wao wa moja kwa moja. Kwa hiyo, kwa kweli nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa taarifa hii. Nina maoni kadhaa kwa malengo mahususi katika dira. Yapo malengo mahususi manne, lakini nitajikita leo kwenye lengo moja tu la maisha bora na ustawi wake kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza dhana ya maisha bora, kama taifa linaloendelea tunatambua yapo maeneo kadhaa ambayo Serikali kwa ujumla wake inapaswa kujikita ili kuinua uchumi wa wananchi kwa ujumla wake. Wizara hii imeonesha mwelekeo na njia ya kupita, ni kazi sasa ya wizara za kisekta kuchukua maono ya wizara hii ya mipango na uwekezaji, kuyachakata na kuyaingiza kwenye mipango ya wizara za kisekta ili yaende yakashamiri na yasambae kwa wananchi kwenye maeneo yote kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye maeneo hayo nilitaka nijikite kwenye maeneo kadhaa. Mfano, tunapozungumzia maisha bora ni lazima uzungumze maisha bora kwa wananchi kwa kutazama miundombinu ya barabara inayozunguka wananchi wale. Katika miundombinu ya barabara lazima tuiangalie kwa nafasi mbili tofauti. Lazima tuangalie barabara zinazosimamiwa na TANROADS, lazima tuangalie barabara zinazosimamiwa na TARURA katika kutekeleza na kupunguza minong’ono na kuimarisha Maisha bora kwa ustawi wa wananchi wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utakubaliana na mimi, kuna baadhi ya meneo mengi sasa barabara imekuwa ni changamoto kubwa sana na Waheshimiwa Wabunge wamesema hapa, zipo barabara ambazo zimetangazwa, wakandarasi wapo site, wanatekeleza, zipo barabara ambazo zimesaini mikataba, wakandarasi hawajaingia site na zipo barabara ambazo zipo kwenye procurement process kwenye maeneo mbalimbali. Lazima tukubaliane kwa kuwa Wizara ya Fedha imesema hapa imetoa mwelekeo wake wa uandaaji wa bajeti, watenge fedha ya namna ya ukamilishaji wa barabara hizi kwenye maeneo yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko barabara ambazo tunazungumzia maisha bora kwa wananchi zimetajwa kwa awamu nne, tano kwenye maeneo tofauti toka miaka ya 95 zinatajwa barabara zile, mpaka sasa tuko mwaka 2025 tunakwenda 2030. Mfano wa Barabara yangu ya Utegi - Shirati kwenda Kirongwe ni matarajio yangu sasa Mheshimiwa Waziri, Wizara ya Fedha itatenga fedha kusaidia Wizara ya Ujenzi ili kuimarisha maisha bora kwenye maeneo yale, ili barabara zile ziweze kukamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara inapokamilika ndiyo inakwenda kuinua uchumi wa eneo husika kwa sababu kuna barabara zinaunganisha kati ya mkoa na mkoa, wilaya na wilaya na zingine zinaunganisha nchi na nchi. Kwa hiyo, katika kuimarisha na kutengeneza maisha bora lazima uweke fedha ya kukamilika kwa barabara ile ili wananchi waweze kupita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni utekelezaji wa miradi ya maji nchini. Niombe sana Wizara husika ya sekta ya maji, ifanye tathmini ijiridhishe badala ya kuwa na tathmini ya namna tumetatua maji kwa asilimia ngapi iangalie upatikanaji wa maji kwenye maeneo yale. Yako maeneo ambayo yana miundombinu ya maji, tunayahesabu kama asilimia katika kutekeleza mpango kazi wa maji, lakini maji hayatoki kwenye maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo wito wangu ni nini, Wizara ya Maji, kwanza ihakikishe miradi ya maji iliyoanzishwa inakamilika, inakwenda, inafika mwisho na inatoa maji. Mbili, wafanye tathmini kwenye miradi ambayo tayari walipeleka miundombinu badala ya kuihesabu kwenye asilimia ya utekelezaji wa maji wajiridhishe kama miradi hiyo kweli inatoa maji na wananchi wananufaika kwenye yale maeneo. Wakifanya hivyo, maana yake watakuwa wanakwenda kwenye ile itifaki ya maisha bora na ustawi wa wananchi kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu ni sekta ya ardhi, hili eneo tumekuwa tukilisahau sana. Kipanga, kupima na kumilikisha tumezungumza kwa mda mrefu sana. Niombe Waziri wa Sekta kwenye awamu hii ya bajeti inayokuja, hili jambo liende lipewe msukumo mkubwa kwa sababu ardhi isiyopangwa na kupimwa kwani ndiyo chanzo cha migogoro ya ardhi kwenye maeneo yetu, maana yake kunakuwa hakuna amani kwenye maeneo yetu. Ardhi yetu inakosa thamani halisi pale inapokuwa haijapangwa, kupimwa na kumilikishwa kwenye maeneo yao. Niombe sana Mheshimiwa Waziri husika, aende alione hili tunapokwenda kuchakata bajeti yake ili waweze kulipa nguvu ili waweze kupata ustawi ulio mzuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, limezungumzwa hapa jambo la soko la vijana, ajira kwa vijana na nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuanzisha Wizara husika ya Vijana, lakini ningeomba sana Waziri husika pamoja na michakato mbalimbali inayoendelea kwenye Wizara hii, lazima waende wakawa-group vijana, tujue hawa vijana wanaowazungumzia ni kuanzia umri upi mpaka umri gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, twende pia tukazungumze fursa sawa kwa hawa vijana kwa kutazama mazingira ya vijana wanayotoka. Kijana wa Rorya mazingira yake kwenye fursa hayawezi kuwa sana na kijana anayeishi Dar es Salaam. Kwa hiyo, Wizara iende ikajikite itazame kama inakwenda kusaidia vijana, isaidie vijana kulingana na mazingira ya maeneo yao wanayotoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, itazame fursa za kimaeneo hayo wanayotoka hao vijana. Tusizungumze general moja kwa moja kwa kuwa-generalize vijana wote kama vile ni sawa kutokana na fursa wanakotoka. Kijana wa Rorya inawezekana fursa yake isiwe sawa na kijana wa Tandahimba, haiwezi kuwa sawa na kijana wa Kinondoni. Kwa hiyo, ni lazima Mheshimiwa Waziri, aende alione hili namna ambavyo anaweza akaliweka ili litengeneze ustawi ulio mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwenye mpango, ni kuhusiana na kilimo. Sisi tunazungumza Mkoa wa Mara, leo hii hatuna zao kuu la kibiashara tunalojivunia, tunazo skim mbalimbali za umwagiliaji pamoja na kuzunguka Ziwa Victoria zaidi ya 70%, hatuna skim kubwa ya kuzungumza leo kama kielelezo cha ukuaji wa kilimo kwenye Mkoa wa Mara. Tunatamani Mheshimiwa Waziri wa Kilimo na mpango huu umekwishaonesha ili waende wakatengeneze upembuzi yakinifu kwenye maeneo yale na sisi tunatamani kupitia mkoa ule tuwe tuna skim ambazo zinawainua wananchi kwenye uchumi na zinaleta manufaa kwenye Wizara hii na kwenye sekta ya kilimo kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana Mheshimiwa Waziri alitazame hili. Mfano, mimi Rorya nimezungukwa na maji 77% lakini ninavyozungumza na wewe hatuna skim yoyote tunayojivunia pamoja na kuzungukwa na maji 77%. Tazama katika 100%, ni 23% peke yake nchi kavu, lakini sina skim yoyote ya umwagiliaji. Kwa hiyo, nikatamani pamoja na kusema, wenzangu wameshauri hapa kuwe na timu ya monitoring and evaluation lakini Wizara ione namna bora ya kusaidia maeneo haya ili waweze kuwasaidia kwenye kilimo, badala ya kubaki na kuzungumza kilimo kwa ujumla wake, lakini maeneo ambayo yana fursa hayanufaiki na kilimo hicho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ningetamani nizungumzie juu ya uchumi wa kimaeneo na Mheshimiwa Waziri amelizungumza sana hapa kwamba, pamoja na kwamba tunakwenda kuunda timu ya monitoring and evaluation lazima tuangalie maeneo hasa ya kimkoa namna yalivyokaa, ni fursa zipi za kiuchumi ambazo zinaweza zikaanzishwa zikawanufaisha mikoa husika. Mkoa wa Mara hatuna mradi mkubwa kama kielelezo kinavyozungumza, hatuna mradi wa skim ya umwagiliaji lakini viwanda tulivyokuwanavyo vyote vimekufa. Matarajio yetu ni nini kutoka kwa Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba, Serikali ione namna ambavyo kama fursa yetu ni kufufua viwanda vilivyokuwepo vikiwemo viwanda vya nguo, kiwanda cha maziwa na fursa zingine ambazo zinaweza zikainua uchumi wa maeneo yale. Ningetamani sana nione Wizara hii na Serikali ikiona namna ya kuweka fedha kuinua mkoa ule. Kwa sababu, ukifanya hivyo kwanza unainua ajira kwa wale vijana, lakini pia watatengeneza uchumi wa mkoa wenyewe husika, kuliko namna inavyokwenda kwa ujumla wake na sisi kama mkoa tunabaki tukiwa bado hatujapata kitu ambacho tunaweza tukasema tunajivunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi na ninasema tena kwa mara nyingine kwamba, ninaunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)