Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Mhe. Dickson Nathan Lutevele (1 total)

MHE. DICKSON N. LUTEVELE aliuliza: -

Je, lini malipo ya waliokuwa wafanyakazi wa Kiwanda cha Karatasi (SPM Mgololo) yatafanyika, ukizingatia kuwa ni ya muda mrefu sana?
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara ninaomba nijibu swali namba 35 kutoka kwa Mheshimiwa Dickson Nathan Lutevele, Mbunge wa Mafinga Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Southern Paper Mills Ltd. (SPM) ilibinafsishwa mwezi Februari, 2004 kwa mwekezaji aitwae RAI Group kutoka Kenya. Baada ya ubinafsishwaji, wafanyakazi wapatao 760 wa kiwanda hicho walifungua Shauri Na.162/2017 la madai katika Mahakama Kuu Tanzania Divisheni ya Kazi dhidi ya Serikali wakidai mafao ya utumishi wao kabla ya kubinafsisha kiwanda hicho. Suala hili la madai ya wafanyakazi hawa bado lipo ngazi ya Mahakama.