MHE. DKT. CHARLES J. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka nipate majibu kwa Naibu Waziri kwamba, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa kituo cha kukusanyia maziwa kilichopo katika Kijiji cha Msomela, Kata ya Misima?
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti ninakushukuru sana. Kadri ya upatikanaji wa fedha ndivyo ambavyo Serikali itaendelea na ujenzi wa kituo hiki cha ukusanyaji wa maziwa kilichopo Msomela. Nakushukuru sana.